Marekani Yamuweka Rais Magufuli Njiapanda......MCC inakutana Kesho Huku Suala La Zanzibar Likiwa Bado Ni Kitendawili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Marekani imeiweka njiapanda Serikali ya Rais Dk. John Magufuli, baada ya Bodi ya shirika lake la Changamoto za Milenia (MCC) kuamua kukutana kesho kujadili masuala kadhaa ya utoaji wa misaada kwa nchi zinazoendelea huku angalizo lake kwa serikali ya Tanzania kuhusiana na uchaguzi wa Zanzibar likiwa bado halijapatiwa ufumbuzi.

Kwa mujibu wa ratiba ya MCC, kikao chao cha Bodi kitakutana kesho (Jumatano) na kupitia mapendekezo ya kupeleka misaada kwa nchi mbalimbali zinazoendelea.

Inaelezwa kuwa kikao hicho kitafanyika kwenye ukumbi wa Holbrooke, saa 4:00 asubuhi kwa saa za Marekani.

Inatarajiwa kuwa kupitia kikao hicho, nchi zitakazokidhi vigezo zitakuwa na fursa ya kuidhinishiwa fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo iliyojipangia yenyewe kabla ya kupata fedha hizo.

Tanzania inasubiri kuidhinishiwa fedha za awamu ya pili za MCC Dola za Marekani milioni 472 (takribani trilioni moja).

Hata hivyo, kutokana na ratiba hiyo, Serikali ya Rais Magufuli inatarajiwa kuwa njiapanda kwani suala la Zanzibar lililokumbushiwa na MCC kupitia maelekezo yake yaliyoripotiwa mwezi uliopita, bado linaonekana kuwa kuendelea kuwa tete.

Hadi sasa, licha ya vikao mbalimbali vinavyoendelea kufanyika na kuwakutanisha wagombea waliokuwa wakichuana kwa karibu kabla ya uchaguzi huo kufutwa, Dk. Ali Mohamed Shein wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Maalim Seif Shariff Hamad wa Chama cha Wananchi (CUF), bado ufumbuzi haujapatikana.

CCM wanaamini kuwa uchaguzi huo ni lazima urudiwe baada ya kufutwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha, huku CUF wakisisitiza kuwa uchaguzi huo haukuwa na kasoro kubwa kiasi cha kufutwa wote na hivyo kutaka matokeo yatolewe na mshindi atangazwe kuwa Rais wa visiwa hivyo.

Awali, katika angalizo lake kwa serikali ya Magufuli iliyoingia madarakani Novemba 5, 2015, MCC ilitaka kupatiwa ufumbuzi kwa suala la Zanzibar na pia kuwapo kwa ufafanuzi juu ya watuhumiwa waliokamatwa kwa makosa ya mtandao wakati wa Uchaguzi Mkuu, Oktoba 25.

Ilifahamika kuwa maelekezo ya MCC kwenda kwa mamlaka mbalimbali za serikali ya Tanzania, yalionyesha kuwa lipo tishio la kufutwa kwa msaada huo (trilioni moja) iwapo mgogoro wa kisiasa wa Zanzibar hautapatiwa ufumbuzi na pia kutolewa ufafanuzi wa sheria ya makosa ya mtandaoni kabla ya kikao cha bodi ya MCC mwezi huu (Desemba, 2015).

 “MCC inafuatilia kwa karibu hatua zitakazochukuliwa na serikali ya Magufuli katika suala la utawala bora, katika kipindi hiki tunapokaribia kufanya kikao cha bodi ya MCC Desemba. Utatuzi wa mgogoro wa Zanzibar kwa kuridhisha pande zote zinazohusika,” ilielezwa katika kile kilichodaiwa kuwa ni sehemu ya angalizo la MCC kwa serikali ya Tanzania na kuripotiwa Novemba, 2015.

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, aliwahi kulitolea ufafanuzi suala hilo  Novemba 29, 2015, akisema kuwa Serikali haina wasiwasi kuhusu mashariti ya MCC juu ya Zanzibar kwani yatafanyiwa kazi kabla ya bodi ya MCC kukutana tena (Desemba).

Hata hivyo, hadi sasa hakuna muafaka uliotangazwa rasmi kuwa umefikiwa kuhusiana na uchaguzi wa Zanzibar huku pande zote zikiendelea kutoa msimamo tofauti; hali hiyo ikielezwa kuwa inaiweka njia panda serikali ya Magufuli kwani fedha za MCC ni muhimu katika utekelezaji wa ahadi zake mbalimbali, hasa juu ya dhamira ya kusambaza umeme na kuwaunganisha wananchi wengi katika gridi ya taifa.

Kadhalika, fedha za awamu ya pili za MCC ni muhimu pia katika uimarishaji wa taasisi zinazohusika na sekta ya nishati.

Akizungumzia hatari iliyopo sasa ya kukosa fedha za MCC baada ya suala la uchaguzi wa Zanzibar kutopatiwa ufumbuzi, Balozi Sefue alisema hakuna hofu yoyote (ya kukosa fedha) kwa sababu tayari kuna hatua kadhaa zimechukuliwa na Serikali ya Tanzania kushughulikia mambo yaliyohojiwa na MCC.

Akieleza zaidi, Balozi Sefue alisema taarifa ya MCC haikusema masuala hayo mawili yaishe vipi, bali walieleza yashughulikiwe; na kwamba hivi sasa yanaendelea kushughulikiwa na yanaendelea vizuri.

Alisisitiza kuwa Tanzania imefuata mashariti yote ya kupata fedha hizo kutoka MCC.

“MCC walituambia sisi kama serikali kuwa yaangalieni masuala haya, na siyo kwamba walituambia tuyashughulikie hadi tuyamalize ndipo watatupatia fedha … hilo siyo kweli,” alisema Balozi Sefue.

Aliongeza kuwa hadi sasa, hatua zilizofikiwa katika kutatua mgogoro wa Zanzibar na pia suala la wahalifu wa makosa ya mtandao, yote hayawezi kuikosesha sifa Tanzania kupata fedha hizo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Wakukaya chapa uwaonyeshe kwamba Tanzania inaweza bila vijisenti vyao
    Fukuza fukuza wote majizi mafizadi filisi malizao
    Haijali wako wapi CCM au upinzani
    Fukuza timua timua viongozi wote walineemeka na mfumo WA kifisadi na wizi

    ReplyDelete
  2. Fanya yako Pombe tuachane na 'omba-omba', hii 'saidia baba' mwisho wata-tutia madole kusiko stahili......

    ReplyDelete
  3. Achana Na vijisenti vyao kwanza kwao huendi Kama alivyokuwa vasco dagama
    Chapa kazi Watanzania tutakukumbuka daima

    ReplyDelete

Top Post Ad