Kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue: Siku 100 za Rais Magufuli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

TAARIFA YA SIKU 100 ZA KWANZA ZA SERIKALI YA
AWAMU YA TANO ILIYOTOLEWA NA
BALOZI OMBENI Y. SEFUE, KATIBU MKUU KIONGOZI,
IKULU, TAREHE 12 FEBRUARI, 2016
__________________________​


Utangulizi
Serikali ya awamu ya Tano imetimiza siku 100 tangu iingie madarakani tarehe 5 Novemba, 2015. Japo siku 100 ni chache sana kufanya tathmini ya kina, zinatosha kuonesha muelekeo wa serikali na kupata kionjo cha uthabiti wa dhamira yake ya kutekeleza ahadi zake kwa wananchi.

Kumekuwa na shauku kubwa ya wananchi kujua kilichofanywa na Serikali hii katika siku zake 100 za mwanzo. Ni shauku ya haki ambayo sisi katika Serikali hii lazima tujaribu tuwezavyo kuikidhi. Ndio maana kuanzia juzi Mawaziri mbalimbali wanazungumzia mafanikio katika hizo siku 100, kila mmoja akienda kwa undani kwenye sekta yake. Nawaomba wananchi wafuatilie kwa karibu yale ambayo Mawaziri hawa wanayatolea taarifa kwenu ikiwa ni sehemu ya uwajibikaji wao kwa wananchi.

Mimi pia, kwa nafasi yangu ya Katibu Mkuu Kiongozi, ambaye ni Katibu wa Baraza la Mawaziri na Mkuu wa Utumishi wa Umma, nimepokea maswali mengi ya waandishi wa habari na wananchi wengine kuhusu siku 100 za kwanza za uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli. Maeneo yanayohusu sekta mbalimbali yatazungumzwa na Mawaziri wanaohusika. Lakini nimeona baadhi ya maswali yanaweza kujibiwa tu na ofisi hii, yaani Ikulu.

Nimeyaweka maswali hayo katika makundi matano na nitayazungumzia kwa ujumla. Yapo maswali yanayohusu uongozi wa Rais wetu, yapo maswali yanayohusu sifa binafsi za Rais wetu, yapo maswali yanayohusu utendaji wake, yapo maswali yanayohusu mahusiano yake na sekta binafsi kwenye utawala wake; yapo maswali yanayohusu mwelekeo wake kwenye mambo ya nje na diplomasia ya Tanzania.

Uongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano Ukoje?
Wahenga walisema, “Nyota njema huonekana asubuhi.” Naam! Katika siku 100 za kwanza, Rais Magufuli amethibitisha kwa uwazi zaidi kuwa yeye ni kiongozi bora na wa kupigiwa mfano. Taarifa tunazoletewa na wananchi ni kuwa kwa kauli, matendo na dhamira yake, wananchi wengi wamemwelewa, wamemkubali na wanamwamini. Katika hizi siku 100, Rais amewathibitishia Watanzania kuwa yeye ni kiongozi, mwenye sifa muhimu za uongozi. Sifa hizo ni pamoja na:
Kiongozi bora lazima awe na dira, maono na malengo kuhusu anakotaka Taifa liende. Katika siku 100 za kwanza Rais Magufuli amedhihirisha kuwa ana sifa hiyo.

Lakini dira bila mkakati ni ndoto. Kiongozi bora lazima awe na mikakati ya kutekeleza dira na maono yake, pamoja na kufikia malengo katika vipindi tofauti. Katika siku 100 za kwanza Rais Magufuli amedhihirisha anayo sifa hiyo.

Kiongozi bora lazima aheshimike na awe na mvuto wa kuwafanya wananchi wamwamini, na kumfuata. Katika siku 100 za kwanza za utawala wake, Rais amewafanya hata ambao hawakumpigia kura, wamwamini, wamwombee na kumfuata.

Kiongozi bora anagawa majukumu, na haogopi kufanya hivyo, lakini anafuatilia. Katika siku 100 za kwanza Rais Magufuli amethibitisha kuwa anayo sifa hiyo.

Kiongozi bora anajua na haogopi kuweka vipaumbele na mpangilio wake wa utekelezaji na kuvisimamia. Katika hizi siku 100 Rais Magufuli amethibitisha anayo sifa hiyo muhimu ya uongozi.
Kiongozi bora haogopi kufanya maamuzi magumu. Hakuna mwenye shaka kuwa katika hizi siku 100, Rais wetu amedhihirisha kwa kauli na kwa vitendo kuwa, anapotetea maslahi ya Taifa na wananchi, haogopi kufanya na kusimamia maamuzi magumu.
Rais ana Maono na Mikakati pevu ya kutimiza maono yake
Kama nilivyosema, sifa mojawapo ya kiongozi bora, ni kuwa na maono pevu na mikakati madhubuti inayote
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad