Nuhu Mziwanda Afunguka ' Shilole Hakuwa Mke Mzuri Kwangu Ndio Maana Nimefuta Tattoo yake'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Msanii Nuh Mziwanda amefunguka baada ya kuachana na mwandani wake Shilole, na kusema kuwa Shilole hakuwa mtu mzuri kwake, ndiyo maana ameamua kufuta hata tatoo ya jina lake aliyoichora.

Nuh ameyasema hayo alipokuwa akiongea kwenye kipindi cha Planet Bongo kinachorushwa na East Africa Radio, na kusema kwamba wakati yupo kwenye mahusiano na Shilole alishindwa kuonesha undani wake, ambao amekuja kuujua baada ya kuachana na penzi kuisha.

“Baada ya mapenzi kuisha mi nimekuwa adui yake, amehack acount yangu ya instagram najaribu kuwacheki wa kurudisha acount yangu wanashindwa kunirudishia anabana kila sehemu, kuna vitu ananifanyia vidogo vidogo ambavyo nimefanya kugundua kuwa hakuwa mwanamke mzuri kwangu, alikuwa anashindwa kuonesha true colour yake nimekuja kuijua baada ya kuachana naye”, alisema Nuhu.

Pia Nuh Mziwanda amesema iwapo wangeachana kwa amani na Shilole asingelazimika kuifuta tatoo hiyo, kwani ni ukweli usiopingika kwamba amemsaidia katika maisha yake.

“Mi ningeiacha tatoo kama Shishi ningeachana nae poa, kila mtu na maisha yake fresh tukionana tunasalimiana hakuna noma, lakini mwenzangu kwenye interviews anasema, akiitwa kwenye interview anaongea hiki kwamba mimi sina kitu, sijui nashindwa kusurvive nakula magengeni, anaongea vitu vingi ambavyo anajaribu kutoa fan base yangu, angekuwa mtu mzuri baada ya kuachana naye tatoo ningeiacha kwa sababu ningejua bado kabaki kuwa rafiki yangu na ni mtu ambaye alinisaidia”, alisema Nuh.

Pamoja na hayo Nuh amesema yeye binafsi hana chuki na msanii huyo ambaye alikuwa naye kwenye mahusiano, na kwa sasa ana mahusiano mengine ambayo asingependa kuyaweka wazi.

Mimi sina ubaya na Shishi , sina ugomvi naye na wala sitaki kufikiria kuja kuwa na bifu naye, nipo kwenye mahusiano lakini siwezi kuweka wazi mahusiano kwenye mitandao ya kijamii, sababu ni mke wangu yuko kwenye moyo wangu, hayupo instagram wala kwenye mitandao ya kijamii”, alisema Nuh.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Huna lolote shombo tu mke unazani ni lelemama? Ujinga tu wa utindio wenu wa ubongo f*****k

    ReplyDelete
  2. kama umeshaoa tulia na mkeo.. sio vizuri kuzungumza mambo ya ex wako. ongea yako na mkeo mpya. japo hayatuhusu ila mnatulazimisha kuyajua.

    ReplyDelete
  3. Akina nuh mpo wengi Tu hpa TZ ,mtt WA kiume unalelewa na unaridhika 2 ndani, huo Ni ujinga kumbuka wao wanahongwa nawe ndio unakula ipo cku utaambiwa ukalipie cjui utatoa Hilo 2ndu, jitumeni acheni umarioo ,mwsho WA cku mnaaibika 2.

    ReplyDelete

Top Post Ad