Chato Yatangaza Kiama cha Mapato

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato mkoani Geita, Batholomeo Manunga amewataka madiwani kuwafichua watendaji wa vijiji wanaoshirikiana na mawakala kuhujumu mapato.

Akizungumza wakati wa kufungua kikao cha baraza la madiwani, Manunga amesema baadhi ya watendaji wa vijiji na kata wanahujumu mapato kwa kula njama na wazabuni.

“Hatutaendelea kuvumilia hali hii, na ni jukumu letu sote kukabiliana na wote wanaohujumu mapato ya halmashauri kwa sababu bila kuongezeka hatutaweza kuwahudumia wananchi waliotuamini na kutuchagua,” amesema Manunga.

Bila kutaja majina wala kata husika, mwenyekiti huyo alisema tayari halmashauri imegundua mtandao wa wanaohujumu mapato ambao wataanza kushughulikiwa baada ya uchunguzi kukamilika.

Amesema watu hao wamekuwa wakiihujumu halmashauri hiyo na kuifanya ishindwe kutekeleza majukumu iliyojipangia kutokana na fedha nyingi kuishia mifukoni mwao.

Manunga aliwasihi madiwani kuacha kuwaonea aibu wezi wa mali za umma ili kuisaidia halmashauri hiyo kupiga hatua kubwa ya maendeleo.

Diwani wa Kata ya Bwina, Sospeter Nyamang’ondi ameishauri halmashauri hiyo kuwachuja mawakala wasiotimiza wajibu na wanaoshirikiana na watendaji kuhujumu mapato.

Amesema iwapo mapato yatasimamiwa vizuri, halmashauri hiyo inaweza kukusanya zaidi ya Sh2 milioni kutoka kwenye mialo.

Diwani huyo amesema mapato mengi yamekuwa yakiishia mikononi mwa watu wachache kutokana na kutokuwapo kwa mikakati mathubuti ya kuwadhibiti.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Athanas Ngambakubi ameahidi kuweka mikakati kuongeza mapato na kubaini vyanzo vipya.

Amewaomba madiwani kushirikiana na watendaji wa halmashauri kubaini vyanzo vipya vya mapato, ukusanyaji na udhibiti wa mapato na usimamizi wa mapato ili kuiwezesha kutekeleza miradi ya maendeleo.

Mkurugenzi huyo amesema bila ushirikiano kutoka kwa viongozi na wananchi itakuwa vigumu kufikia malengo.     

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad