Idadi Ndogo ya Wapiga Kura Wajitokeza Uchaguzi wa Marudio Zanzibar.....

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Zanzibar Uchaguzi Mkuu wa marudio wa Zanzibar umefanyika kwa amani na utulivu huku kukiwa na idadi ndogo ya wapiga kura, ikilinganishwa na idadi ya waliojitokeza katika uchaguzi uliofutwa wa Oktoba 25, mwaka jana.

Takwimu za Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), zinaonyesha kuwa waliojiandikisha kwenye Daftari la wapiga kura kwa Unguja na Pemba ni 503,860, na sehemu zote hizo zilikuwa na jumla ya vituo vya kupigia kura 1,580, na  kila kituo kina wastani wa wapiga kura 350.  

Katika uchaguzi huo vyama vya CCM, AFP,  ADC  na CCK vimeshiriki katika uchaguzi huo na kuweka mawakala wake vituoni huku chama cha CUF kikiwa hakina wakala yeyote kwenye vituo  vyote vya kupiga kura vya kisiwani Unguja.

Pamoja na kuwepo kwa hali ya taharuki katika siku za karibuni visiwani hapa, hali hiyo imekuwa tofauti ambapo leo  maeneo mengi yalionekana kuwa na amani, pia vikosi vya ulinzi havikujitokeza barabarani kama ilivyozoeleka.

Maduka mengi yalionekana kufungwa na katika vituo vya kupiga kura ambavyo inadaiwa  ni ngome ya CUF, watu walijitokeza kwa idadi ndogo ikilinganishwa na wale waliojitokeza kwenye maeneo ambayo ni ngome ya CCM.

Katika Kituo  cha Shule ya Sekondari Bububu pamoja na msimamizi wa kituo hicho Mohammed Zamani,  kusema kuwa watu walijitokeza kwa wingi kupiga kura, wakala wa chama cha AFP, Fumo Machano Fumo alieleza kuwa tokea kufunguliwa kwa kituo hadi sita mchana watu waliokuwa wamepiga kura katika chumba chake walikuwa 25.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad