Watu Wanne Watiwa Mbaroni Kwa Tuhuma za Kutumia Jina la Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Kutapeli

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Watu wanne wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na tuhuma za kujipatia fedha kwa kutumia jina la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

Washtakiwa hao walifikishwa katika mahakama hiyo jana kujibu mashtaka 12 yanayowakabili, likiwamo la kughushi barua na kuziwasilisha katika vituo vya mafuta wakirubuni watumiwe kiasi cha fedha ili waweze kupata punguzo la kodi.

Washtakiwa hao ni mwanafunzi, Issa Mohamed Awadhi (27)
maarufu kama Charles Robert au Mwamunyange, mkazi wa Ilala, ambaye hakuwapo mahakamani hapo kutokana na kulazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) baada ya kuugua.

Wengine ni Hamisi Tembo(37) mkazi wa Ilala, mtengeneza mihuri, Nicolaus Obado(32), mkazi wa Mbagala Kuu na Wakati Mungi (51) mfanyabiashara na mkazi wa Yombo Makangarawe.

Washtakiwa walikana mashtaka na upande wa mashtaka ulidai upelelezi haujakamilika na kukosa dhamana. Kesi itaendelea Aprili 11
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad