Mahakama ya Kisutu Yafuta shtaka la Kutakatisha fedha dhidi ya Aliyekuwa bosi wa TRA, Harry Kitilya na wenzake Wawili

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Kisutu jijini Dar es Salaam, leo imefuta shtaka la utakatishaji fedha (money laundering) lililokuwa likimkabili Kamishna Mkuu Mstaafu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya sambamba na waliokuwa wafanyakazi wa Benki ya StanBic Tanzania, Sioi Sumari na Shose Sinare.

Awali watatu hao walikuwa wamenyimwa dhamana. Kutokana na uamuzi huo, mawakili wao sasa wanaweza kuwaombea dhamana.

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), iliwafikisha mahakamani watatu hao April 1, kwa kisa la:- Kula njama na kujipatia kwa udanganyifu kinyume na kifungu Na. 384 cha Kanuni ya Adhabu (Cap 16 R.E. 2002) ; Kughushi kinyume na kifungu Na. 333,335 (a) na 337 cha Kanuni ya Adhabu (Cap 16 R.E 2002) ; Utakatishaji wa fedha haramu kinyume na kifungu Na. 12 (a) 13 (a) cha Sheria ya ya Utakatishaji fedha Na. 12 ya Mwaka 2006 ‘Anti- Money Laundering Act’.

Watuhumiwa hao walidaiwa kufanikiwa kujipatia fedha kwa njia ya kughushi dola milioni 6, kama malipo ya kufanikisha serikali ya Tanzania kupata mkopo wa dola milioni 550 kutoka Benki ya Stanbic ya Jijini London mkopo ambao ulipitia benki ya Stanbic tawi la Tanzania.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Haya ndo majipu yanapeta na mablions of dolla
    Tanzania wacha

    ReplyDelete
    Replies
    1. Halafu eti tunajiita maskini.

      Delete

Top Post Ad