Ajipiga Risasi Akitafuta 'Selfie ya Mwaka'

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Polisi India wamesema kuwa kijana mmoja amejipiga risasi kichwani kimakosa,akitafuta mbinu ya kujipiga picha ya ''selfie'' ya kipekee akiwa na bastola ya babake.

Kijana huyo mwenye umri wa miaka 15 anaendelea kupokea matibabu katika hospitali kuu ya Pathankot iliyoko katika jimbo la Punjab

 Yamkini ajali hiyo ilitokea ijumaa jioni kijana huyo aliporejea nyumbani akitoka shuleni .
Walioshuhudia wanasema kuwa alichukua bastola ya babake iliyoidhinishwa na serikali lakini kwa bahati mbaya akajipiga risasi kichwani akitaka kupiga selfie akiwa ameshika bastola kichwani.

Tukio hilo limevutia hisia kali miongoni mwa wenyeji ambao bado wanaomboleza kifo cha kijana mwengine aliyekanyagwa na treni akijaribu kupiga selfie kwenye reli huku gari moshi likija kwa kasi.

Takriban nusu ya idadi ya vifo vya watu 27 vilivyotokea kote duniani mwaka wa 2015 kutokana na picha za ''selfie'' vimetokea nchini India
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad