Haya Hapa Matokeo ya Simba na Azam Yaliyofanya Mashabiki wa Yanga Waendelee Kuchekelea Kileleni...

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ligi Kuu soka Tanzania bara imeendelea leo Mei 1 2016 kwa mchezo kati ya Simba dhidi ya Azam FC kuchezwa katika uwanja wa Taifa Dar es Salaam, huu ni mchezo wa 26 kwa vilabu vyote na ulikuwa mchezo muhimu kwa kila klabu hili kujiweka pazuri katika nafasi ya kuwania ubingwa.

Azam FC kabla ya mchezo dhidi ya Simba kumalizika kwa sare ya 0-0 walikuwa na point 58 wakiwa nafasi ya pili ya Ligi, wakati Simba walikuwa nafasi ya tatu wakiwa na point 57 wakiongozwa na Yanga ambao wapo kileleni wakiwa na point 65 na michezo 26. Sare ya mchezo huu ilikuwa ni furaha kwa Yanga ambao wameongeza tofauti ya point kwa Azam FC na Simba.

Kwa idadi ya mechi Simba na Azam FC huu ulikuwa ni mchezo muhimu kwao kuhakikisha wanapata point tatu ili kuweza kupunguza tofauti yao ya point na Yanga wanaoongoza Ligi wakiwa na tofauti ya point sita na Azam FC anayefuatia, umuhimu wa mchezo kwa pande zote mbili ndio ulifanya mchezo kuwa na tension kubwa kitu ambacho kilifanya wachezaji wa pande zote kukosa magoli ya wazi wakati mwingine.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. YANGA BIGWAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAAA

    ReplyDelete

Top Post Ad