Godbless Lema Amnyooshea Kidole Mwigulu Nchemba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

WAKATI  Rais Dk. John Magufuli akitarajiwa kumwapisha Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, Ikulu, Dar es Salaam leo, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema) amemnyooshea kidole waziri huyo.

Kupitia taarifa yake   kwa vyombo vya habari jana, Lema ambaye ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani, alisema  wizara hiyo ni nyeti na muhimu kwa usalama wa taifa  hivyo Mwigulu anapaswa kuwa makini, mwangalifu na mwenye utulivu.

“Ni heshima kubwa uliyopewa na Rais, unapaswa kuwa makini, mwangalifu na mwenye utulivu. Natarajia   jambo la kwanza utakalofanya ni kutambua kuwa  na wingi wa silaha za kisasa kwa askari wetu si suluhisho la ulinzi na amani katika taifa letu, bali haki na matumaini ya wananchi ndiyo msingi madhubuti wa amani na utulivu wa nchi.

“Polisi wetu na askari magereza wanaishi maisha magumu, mishahara haitoshi  wanahitaji uelewa wako juu ya maisha yao na kazi zao.

“Umeteuliwa wakati  Serikali kupitia jeshi la polisi inatumia nguvu zote kukandamiza na kuangamiza demokrasia.

“Vyama vya siasa vimezuiwa kufanya mikutano ya hadhara nchi nzima kwa sababu ambazo hazina msingi wowote kinyume cha sheria na Katiba ya nchi, huku pia uhuru wa maoni, habari na taarifa ukiwa shakani,” alisema.

Alisema taifa linatarajia Waziri Mwigulu atakuwa  mshauri mzuri wa Rais  Magufuli kuhusu masuala hayo pamoja na wajibu wa polisi katika demokrasia kwa sababu  kuitia  shaka demokrasia ni kuharibu ustawi wa jamii nchini.

Alimshauri  Mwigulu  kutafuta waraka wa hotuba ya kambi ya upinzani kwa wizara hiyo iliyozuiliwa kusomwa bungeni kwa sababu ina mambo mengi ambayo yanaweza kumsaidia.

“Kuna mambo mengi tulilieleza katika hotuba  yetu… ni vema ukaitafuta hotuba hiyo na ukatazama kwa makini mambo ambayo yalizuiwa kusomwa na uone namna utakavyowajibika juu ya mambo hayo.

“Hapo ndipo unapaswa kuanzia. Na wananchi wanasubiri kukupima katika hilo.

“Hata hivyo, ninakutakia kila la heri katika wajibu wako huu mpya, ninafahamu changamoto  za wizara hii hasa wakati huu ambao mauaji ya binadamu  na ugaidi ni tishio duniani na Afrika Mashariki,” alisema.

Pamoja na kumwapisha Waziri Mwigulu leo, Rais Magufuli pia anatarajiwa kumwapisha Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Charles Tizeba.

Kabla ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu ndiye alikuwa Wazira wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. hongera mwigulu lakini kaza sana

    ReplyDelete
  2. Hataiweza hii kazi. Hapa Magufuli kaburunga. Hujui wadhifa wa hiki miti kuweka mjomba. Hivi Twiga mnalipeleka wapi Ccm. Nchemba hii kazi mzigo hana wezi nayo. Hivi ndugu magufuli u po serious.unakatisha Tamaa ya wananchi waliokuchagua.hapa umeshindwa.

    ReplyDelete

Top Post Ad