AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Waraka huo ulijikita katika maagizo ya Jeshi hilo kupiga marufuku mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa pamoja na kuwashikilia na kuwahoji viongozi wa vyama hivyo akiwemo mwenyekiti wake, Freeman Mbowe hivi karibuni.
Lowassa alimueleza IGP kuwa amelazimika kumuandikia barua hiyo ili kuweka kumbukumbu sahihi baada ya kupata taarifa za kuzuiwa kwa viongozi wa Chadema kufanya mikutano wakati yeye alipokuwa nje ya nchi.
Alihoji sababu za kiintelijensia zinazotolewa na jeshi hilo kuzuia mikutano hiyo kwa madai kuwa limebaini kuna uwezekano wa kutokea vurugu zimetumika ili kuhalalisha uminywaji wa demokrasia ya vyama vya siasa kwani hata historia inaonesha vinginevyo.
“Uzoefu wa historia unakinzana na madai hayo, kwa sababu yako matukio mengi ambayo yamethibitisha kwamba mijumuiko ya wanasiasa wa vyama vya upinzani, yakiwemo maandamano na hata mikutano ya hadhara yamefanyika kwa amani,” alisema.
“Iko mifano mingi inayoonesha kwamba tumefanya shughuli mbalimbali za siasa kwa maana ya maandamano na mikutano ya hadhara kwa amani na pasipo kuwapo hata ulinzi wa polisi,” alisema Lowassa kwenye waraka huo.
Alisema kuwa sababu hizo ndizo zinazopelekea wao kupinga maagizo hayo ya polisi ya kuzuia kufanyika kwa mikutano kwa kuwa sababu za kiintelijensi zinatumika kama kichaka cha misukumo iliyo nyuma ya maagizo hayo.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
anasaini kitabu cha maombolezo au anaandika barua?
ReplyDeleteHiyo ni picha tu jamaa...
Deletemwandishi nenda shule
ReplyDeleteAhhh!! Lowassa wewe Si uligonbea kiti cha Uraisi Na unaweza kuandika hivi!! Tutaaninije Kama ndiyo wewe?? Maanake Ni utumbo Na hakuna maintiki wala Uzalendo au kwa ajili ya heshimma waliokupa sasa unalipa fadhila zao???? Lowassa hwbu rudia kuisoma Na ujiulize wananchi wataipokea vipi?? Maanake Mimi nakushangaa!!
ReplyDeletekweli wewe Lowassa mimi nilikuwa nakuona umewiva.. lakini 😎 hapa umechemsha na haii ingii akilini ila kama una fikiria kuwa Dj Mbowe ataona hauumpi tafu wakati kama huu hapo tunaweza kukuelewa kwamba unalimda masilahi yako ya kibinafsi..au sivyo???? Inasikitisha
ReplyDelete