AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kwa mujibu wa taafia iliyotolewa leo na Mkurugnezi Mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara imesema hatua ya kuwasimamisha kazi wakurugenzi na mamenja hao inafuatia kikao cha bodi chini ya uenyekiti wa Prefesa Samweli Wangwe kilichokaa kuanzia Ijumaa iliyopita.
“Bodi imeagiza kusimamishwa kazi Wakurugenzi , Mameneja watano na Mhandishi mmoja ili kupisha uchunguzi ili kubaini wahusika katika tuhuma za ubadhirifu, matumizi mabaya ya ofisi na kutofuata kanuni, sheria na utatibu katika uwekezaji, usimamizi wa miradi na manunuzi ya ardhi na ajira,” alisema Profesa Kahyarara.
Aliwataja wakurugenzi hao ni Mkurugenzi wa mipango, Uwekezaji na Miradi, Yakub Kidura, Mkurugenzi wa fedha, Ludovick Mrosso, Mkurugenzi wa rasilimali watu na utawala, Chiku Matessa, Mkurugenzi wa Udhibiti,Hadhara na Majanga, Sadi Shemliwa, Mkurugenzi Mahesabu ya ndani, Pauline Mtunda na Mkurugenzi wa Uendeshaji, Crescentius Magori.
Aidha Aliwataja mameneja waliosimamishwa ni pamoja na Meneja wa utawala, Amina Abdallah, Meneja wa Uwekezaji, Abdallah Mseli, Meneja Miradi, Mhadisi,John Msemo, Mhasibu Mkuu, Davis Kalanje, Meneja kiongozi mkoa wa Temeke, Wakili, Chedrick Komba na Mhadisi John Ndazi.
Awali amedaiwa kuwa baadhi ya wakurugenzi na mameneja waliosimamishwa, leo wamefikishwa katika kituo cha polisi cha kati Dar es Salaam kwa mahojiano kufuatia tuhuma hizi zinazowakabili.
a wakurugenzi wote wa NSSF wamepigwa chini leo na wanne kati yao wako chini ya ulinzi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Wajibika kiuadilifu Na uaminifu..vinginevyo hatutaelewana..hasa kiujanja ujanja
ReplyDeleteEeeh safi sana,ukilima matembele utavuna matembele.Wizi huleta
ReplyDeletemaringo,uchoyo,ujeuri,ndivyo wengi kati ya hao walivyokuwa kumbe dhambi ya kuiba ndio ilikuwa inazaa yote hayo.Sio wote,lakini watakaowajibishwa wala msiwe na shaka kuna mahakama ya mafisadi yaani ni nzuri kweli kwa ajili yenu.
Mmmh,yaani wewe!
Delete