GEITA: Waziri Mwigulu Aweka Gwaride la Utambuzi, Amkamata Mchina Aliyemtesa Mtanzania

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Nimefika Mgodi wa Nyamhuna unaodaiwa kuwa raia wa china ambao ni sehemu ya wamiliki wa mgodi huo wakishirikiana na watanzania walimtesa kinyama na kumjeruhi mmoja wa mtanzania mwenzetu aliyekuwa akifanya kazi katika mgodi huo uliopo Katoro-Geita.

Imenilazimu kufika gereza la Geita kukutana na kijana huyo ambae yupo hai tofauti na taarifa za awali kuwa alifariki.Baada ya kujiridhisha kuanzia mavazi,majeraha,picha,sura na umbo lake kuwa ndiye kijana aliyeteswa vibaya na picha zake kusambaa mitandaoni na vyombo mbalimbali vya habari,niliamua kwenda naye hadi mgodini lilipofanyika tukio hilo la kinyama,aliwatambua wahusika ambao NI KWELI WALIFANYA TUKIO HILO LA KINYAMA NA LISILOKUBALIKI HAPA NCHINI.

Hivyo walioshiriki tukio hilo tumeshawashikilia kupitia jeshi la polisi tayari kwa kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Nalaani tukio hilo vikali sana,serikali hii ipo tayari kushirikiana na kila mmoja rai mwema kutoa taarifa popote pale za matukio au viashiria viovu na vinavyohatarisha usalama wetu.

"Usalama wetu,jukumu letu sote"

Copy and Paste from Mwigulu Nchemba Facebook Wall

My take
Huu Unyama unaofanywa na Raia wa Kigeni hapa Nchini kwetu unatakiwa kuchukuliwa kwa hatua kama hizi tena haraka sana iwezekanavyo. Mijitu isiyokuwa na Huruma pamoja na Kumtesa kwa kumsurubu Mtanzania mwenzetu, bado haikutosheka Ikambambika kesi na kumsweka Lupango ndugu yetu huyu.

Haya hayafanywi tu huko Migodini, Hata hawa Wahindi wanawanyanyapaa sana Dada zetu wanaofanya kazi za Nyumbani kwenye Makazi yao. Serikali inapaswa kupanua jicho kuangalia wananchi wake wanavyonyanyapaliwa na hawa wageni huku wao wakiishi kama wako kwao.

Heko Mwigulu Nchemba.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

13 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Heko waziri wetu kwa kutujali watanzania, Magufuli hakukosea kukuteua

    ReplyDelete
  2. Mimi si CCM
    Nawapenda mawaziri Kama hawa wanaofuatilia mambo
    Asante waziri
    Asante Magu
    Nafikiri CCM mtaanza kujifunza
    Wazee kama wasira hawaendani na wakati
    Kwanza si watu wa social network
    Bravo mnyapaaa Mwigulu

    ReplyDelete
  3. Wapo watakaokupuzia
    Watakaotukana
    Wazushi
    Waongo
    Lakini yapo ya ukweli pia hapa
    Nape mdogo wangu fungua zaidi uhuru wa habari na utandawazi

    ReplyDelete
  4. Tena Mwigulu na hao polisi walio mtia ndani ndugu yetu fukuza pamoja na hakimu pia

    ReplyDelete
  5. Hata magufuli anasoma hii mitaandao
    Kwani kuna mengi ya kujifunza hapa

    ReplyDelete
  6. Nakupongeza Mheshimiwa Mwigulu kwa kazi nzuri, wawekezaji uchwara wa aina hii ni wengi. Nina uhakika huu ni mwanzo tu wa ufuatiliaji mzuri wako wa mambo mengi maovu wanaofanyiwa wananchi wanyonge wanaopeteza haki zao za msingi, kisa hawana fedha. Ushauri wangu kwako Mwigulu, angalie kwa jicho la tatu idara ya polisi, mengi utayaona ya wananchi kunyimwa haki zao za msingi. Mungu akutangulie kwa kazi nzito ulionayo mbele yako.......

    ReplyDelete
  7. Nakupongeza Mheshimiwa Mwigulu kwa kazi nzuri, wawekezaji uchwara wa aina hii ni wengi. Nina uhakika huu ni mwanzo tu wa ufuatiliaji mzuri wako wa mambo mengi maovu wanaofanyiwa wananchi wanyonge wanaopeteza haki zao za msingi, kisa hawana fedha. Ushauri wangu kwako Mwigulu, angalie kwa jicho la tatu idara ya polisi, mengi utayaona ya wananchi kunyimwa haki zao za msingi. Mungu akutangulie kwa kazi nzito ulionayo mbele yako.......

    ReplyDelete
  8. Hongera sana mh waziri, safi sana, hao wachimba migodi wanadharau sana watanzania.

    ReplyDelete
  9. KWA HILI MWIGULU NAKUFAGILIA SANA. HAWA WATANZANIA WAKIASIA WANATESA SANA DADA ZETU NA KAKA ZETU WANAOWAFANYIA KAZI HILI LIWE FUNDISHO KWAO . JAMANI KAMA UNANYANYASWA USIKA KIMYA SEMA HATA KAMA NI MTANZANIA MWENZIO SEMENI JAMANI HEKO MWIGULU NCHEMBA!!!

    ReplyDelete
  10. CONGRATS MHE. WAZIRI MWIGULU. HAKIKA VIJANA TUNAWEZA. HEKO HEKO RAIS WANGU JPM KUMTEUA WAZIRI HUYU. HAKIKA MUNGU YUKO NAWE. WATANZANIA TUKO NAWE BEGA KWA BEGA KUFANIKISHA AZMA YAKO YOTE KATIKA UTAWALA WAKO NA SERIKALI. USIOGOPE TUNAKUOMBEA.

    ReplyDelete
  11. Asante kwa kujali,hii inaonyesha ni jinsi gani watu weusi tunadhalauliwa na hii mijitu kwenye ardhi yetu kwa kuutumia unyonge na umaskini wetu,hao wahindi ndio usiseme,na kubaka dada zetu wanabaka.Kesi ikiisha warudishwe kwao pumbavu hawa.

    ReplyDelete
  12. Siri ya Wachina. Wabaguzi, Hawatii amri mpaka uwachape viboko, Hawathamini binadamu yeyote ila mchina mwenzake. Kwa nini Serikali ya Kikwete inawaleta vibarua Wachina Tanzania. Kwa nini serikali ya CCM inawaleta na kuwaruhusu Wachina wasio na elu kuja kufanya kazi migodini, Kwa nini Tanzania kwa miaka kumi imeruhusu Tanzania na mali nyingi imilikiwe na Wachina. Wachina Wengi hawana ustaarabu. Wachina wengi kama hawa ni maskini wa mwisho nchini kwao.Kazi zote za uchimbaji zifanywe na Watanzania. Wachina Tapeli, Wachina wanaingiza bidhaa chafu makopo na Wachina wauaji tembo, na Wauza meno. Kunasehemu za nchi Mchina asiingie kwa manufaa ya nchi hii. Mikataba yote ya Wachina ni mibovu kwa nchi. Viongozi waliopita ndio walioruhusu hii mikataba mibovu.Ni hawa viongozi inabidi Watumbuliwe kwa kushindwa kusimamia haki, kutokulinda maslahi ya watu na mali za Watanzania. Ni hawa polisi wanaowanyanyasa Watanzania wenye nchi hii kwa kuchekelea na kumruhusu Mchina afanye ujambazi, ujangili, na unyanyasaji. Polisi kama hawa ni weni wametanda nchi nzima. Si waadhibiwe tu, wafukuzwe kazi na kufungwa. Wanambambikizia kesi kijana ambaye ashaharibiwa maisha yake na kumweka ndani. Rushwa imetembezwa na wachina kuwapa vijisenti polisi wakijua hawalipwi vizuri. Wananchi amkeni muwe na kamera simu tayari kurekodi uonevu huu.Tanzania si shamba la wachina na viongozi wachache walioenda ubia nao kupitia nyazfa zao. Mnawajua watoto wa madingi wamiliki, mbona mnawaonea haya. Mnajaribu kwa kila njia kuwatetea kuwazibia . lakini kila kukicha jingine linajichomoza. Fukuza Wachina wpote wenye ubia na vigogo wanaoruhusu mtanzania kijana kama huyu kunusurika maisha. Huenda huyu kijana ni peke yake tegemezi kwa familia nzima. Mnaokwamisha utumbuaji nchini matokeo ndio haya. namshukuru Nchemba, lakini namuomba Nchemba pia asimamie haki ya Watanzania walio wengi kwanza. Naomba Watanzania wote msiridhike, fuatiliani kwa undani kuhusu hukumu ya huyu mtu. Wachina Wanawanyonga Watanzania nchini kwao. Machina ni hatari kuyajanza Tanzania na Afrika. Watachukua kila kona, kila mali, na Mchele mwingi unaoletwa Africa umetengenezwa na plastic. Wengi Waafrica watakufa.
    Kama nasema uongo pimeni aina zote za mchele toka Uchina. Kwa mchina mwafrika ni mnyama. Lakini atacheka akuchote akili mpe kila siri ili tu akusafisha mpaka uvunguni.

    ReplyDelete
  13. Nakuomba Waziri nchemba weka simu ili watu wapige simu na bila kujitambulisha au kuwachukulia hatua ili watoe ukweli wa wachina , majambazi, na mafisadi. Ni hivi tu Watanzania mtajikwamua kutokana na hawa watu, Wawekezaji. Awe mhindi, mzungu, mfaransa, iwe sehemu ya kuripoti haya mambo kwa kweli. Tumedharalika vya kutosha.

    ReplyDelete

Top Post Ad