Lulu Usitukane Wakunga, Uzazi Ungalipo!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

KWAKO mtoto mzuri ndani ya Bongo Muvi, Elizabeth Michael ‘Lulu’. Hujambo? Habari ya huko ulipo? Wazima wote na familia yako? Shemeji yetu naye hajambo? Hongera maana naona siku hizi umeamua kumuanika hadharani.

Ukitaka kujua afya ya mimi kaka yako, sijambo. Namshukuru Mungu, naendelea kupambana ndani ya mjengo wa magazeti Pendwa, Global Publishers Ltd. Hapa sisi ni kazi tu!

Nimekukumbuka leo kwa barua. Kitambo kidogo sijakuona. Siku hizi umekuwa mzito sana kuzurura kwenye viwanja vyetu vya kujidai. Sikulaumu katika hilo, huenda ni utaratibu mpya ambao mwenyewe umejipangia. Ni jambo zuri pia. Staa anapaswa kupotea kidogo siyo kila kiwanja awepo.

Historia ya maisha yako inaonesha umeweza kukutana na changamoto nyingi ambazo naamini zilikuwa kubwa kuliko umri wako. Umejitahidi sana kuzikabili na maisha yanaendelea vizuri, mshukuru Mungu pia kwa hilo. Si akili zako bali ni kwa neema na rehema zake.

Madhumuni ya mimi kukuandikia barua hii, nina jambo. Nataka kukumbusha kwamba; usitukane wakunga wakati uzazi ungalipo. Sikufurahishwa na kitendo cha wewe kuwatukana waandishi wa Global Publisher hivi karibuni.

Wewe na vyombo vya habari (hususan Global) ni kama chanda na pete. Ukubali ukatae, magazeti yake yamechangia kwa kiasi kikubwa sana kukufikisha ulipo leo. Hata kama yanauza kupitia habari za mastaa lakini mchango wake katika maendeleo yenu ni mkubwa.

Kwa kuandika habari zako, zimesaidia kwa kiasi kikubwa kuwashawishi Watanzania kukufuatilia. Kujua unafanya nini kwa wakati husika na kisha kukusapoti kwa kununua kazi zako.

Hata pale ulipopata majanga mbalimbali, kama kampuni kwa namna moja au nyingine iliweza kutoa mchango wake. Hata usipokiri hilo hadharani, lakini moyoni unajua. Siwezi kufafanulia kila kitu lakini ukweli unaujua.

Katika hilo si wewe tu, hata familia hususan mama yako anajua mchango wa Global katika maisha yako. Haujavuka mto kiasi cha kutukana mamba. Unaanzaje kuwatukana waandishi wa Global? Ujasiri huo unautoa wapi? Mafanikio gani yanayokupa jeuri?

Unawatukana waandishi wa kampuni ambayo unajua imekutoa wapi kweli? Kwani ukiwapa majibu ya kwamba hilo siwezi kulizungumzia, utapungua nini? Hujisikii kuongea, unaweza ukakaa kimya, hakuna atakayekulazimisha. Maana misingi ya habari inatoa nafasi kubalansi, ukiwa hautaki wao wanajua nini cha kufanya.

Global ina watu wanaokuzidi umri mara tatu au nne. Kuna wafanyakazi ambao wanaweza kukuzaa, unapata wapi ujasiri wa kuwatukana? Unaweza kumtukana mtu aliye sawa na umri wa wazazi wako? Au unataka kutuaminisha kwamba huwa unafanya hivyo kwa wazazi wako? Naamini jibu ni hapana, sasa kwa nini ufanye hivyo kwa watu ambao unajua wana umri sawa au zaidi ya wazazi wako?

Mdogo wangu nataka uelewe kwamba ulikosea, unapaswa kuomba radhi. Hupaswi kuwavimbia kichwa waandishi wa habari wakati haohao bado utawahitaji huko mbeleni. Haohao wanaweza kukusaidia jambo kubwa sana pengine huko uendako.

Nakushauri kuwa muungwana, omba radhi na maisha yataendelea kama kawaida. Kwa umri wako hauna sababu ya kuweka bifu na waandishi wa habari, si wa Global tu hata wa vyombo vigine vya habari. Unahitaji sapoti yao ili uweze kusonga mbele.

Yangu mimi ni hayo tu kwa leo, ni matumaini yangu utakuwa umenielewa na utatumia busara katika hili. Mungu akusimamie!

Mimi ni kaka yako;

GPL

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Yani sheria hairuhusu kutukana na mm ningewatukana kwani nyie waandishi mnavyoandika habari za uongo na za uzushi wakat mwingine huwa mnamuuliza nani mi sio shabiki wa lulu lakn nyie global siwapendiii nyie na bosi wenu..hv mnajionaga nyie ni miungu watu au kipindi kile mliisakama ze komedi wee haya kiko wapi sio hao wanaendelea...kwani msipomuandika anapungukiwa nn kwanza ndo vzr utamuepusha na mengi ili akili yake nae itulie kuliko kuandamwa kila saa...mlimsakama uwoya akawatolea mbovu mkajidai kumpa promo batuli kwamba mkavimbia uwoya hamuandiki habari zake alipungukiwa na nn labda acheni hizo nyie..huyo bosi wenu kujifanya wa din wakat ni mnafki no wonder hakuna anayesoma hizo takataka mnazochapisha now days.....achen kufuatilia maisha ya wenzenu na kuwatisha ooh sijui tulikufanyia nn kama ulifanya wema kwake nenda zako unasubir akushukuru habar zenyewe mnasubir wapost inst ndo mmchukue muandike...acheniii watoto wa watu mmezidi nyue aaah..

    ReplyDelete
  2. Yani sheria hairuhusu kutukana na mm ningewatukana kwani nyie waandishi mnavyoandika habari za uongo na za uzushi wakat mwingine huwa mnamuuliza nani mi sio shabiki wa lulu lakn nyie global siwapendiii nyie na bosi wenu..hv mnajionaga nyie ni miungu watu au kipindi kile mliisakama ze komedi wee haya kiko wapi sio hao wanaendelea...kwani msipomuandika anapungukiwa nn kwanza ndo vzr utamuepusha na mengi ili akili yake nae itulie kuliko kuandamwa kila saa...mlimsakama uwoya akawatolea mbovu mkajidai kumpa promo batuli kwamba mkavimbia uwoya hamuandiki habari zake alipungukiwa na nn labda acheni hizo nyie..huyo bosi wenu kujifanya wa din wakat ni mnafki no wonder hakuna anayesoma hizo takataka mnazochapisha now days.....achen kufuatilia maisha ya wenzenu na kuwatisha ooh sijui tulikufanyia nn kama ulifanya wema kwake nenda zako unasubir akushukuru habar zenyewe mnasubir wapost inst ndo mmchukue muandike...acheniii watoto wa watu mmezidi nyue aaah..

    ReplyDelete

Top Post Ad