AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Tayari baadhi ya wakuu wa mikoa na wilaya nchini wamekutana na viongozi wa makanisa kuwaomba waambie waumini wao wasitoke kuandamana na kwenye mikutano ya hadhara ya Chadema.
MwanaHALISI online limefanikiwa kuona barua za kutoka wilaya kadhaa kwenda kwa viongozi wa dini ambazo zilielekeza kufanyika vikao katika ofisi za wilaya kati ya tarehe 22- 23 Agosti 2016 ajenda kuu ikiwa ni kuwashauri viongozi wa dini wawatangazie waumini wao kuwa UKUTA ni sawa na uvunjifu wa amani.
Wakuu wa wilaya hao wamewaonya viongozi wa dini kuwa kama wafuasi wao wataandamana itakuwa ni sawa na viongozi wa dini kushiriki maandamano na mikutano ya hadhara.
Waraka wenye kumb Na.ab.214/433/01 “B” 03 ya Agosti 18 mwaka huu, iliyosainiwa na Kaimu Rozalia J Njiani, Katibu Tawala wa Wilaya ya Karagwe ambayo MwanaHALISI online limeiona ni moja kati ya nyaraka nyingi zilizosambwazwa kwa viongozi wa dini nchini
Viongozi wa dini wameonekana kukasirishwa na uamuzi huo wa serikali lakini baadhi yao wamenukuliwa wakitoa msimamo dhidi ya wito huo wa serikali.
MwanaHALISI online limefanikiwa kuona kiongozi mmoja wa dini akimwandikia mwenzake kuwa “Muda wote tumekuwa kiunganishi kwa vyama vyote. sauti ya kinabii ilibaki pale pale inapotakiwa kuwa hata kama Kanisa lilionekana kuegamia upande mmoja, sheria za nchi ni lazima ziheshimiwe na katiba ya nchi iheshimiwe ndio msimamo wa sisi viongozi wa dini, hatutatetereka.”
Haya yanajiri ikiwa ni muda mchache tangu ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa kutangaza kuvikutanisha vyama vyote vilivyojiandaa kufanya maandamano vikutane katika meza ya mazungumzo.
Ukuta ulitangazwa kama azimio la Kamati Kuu ya dharura ya Chadema iliyoketi tarehe 23-26 Julai, 2016 kujadili hali ya siasa na uchumi wa Taifa tangu serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani mwezi Novemba, 2015.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Kwa hili msiwape shida viongozi wa dini Kabisa
ReplyDeleteWatu huenda kanisani au msikitini kuomba mungu na wala siasa
Ongeeni nyinyi wenyewe wana siasa
Mungu ibariki Tanzania
UONGO WA BARUA ZA KUTENGENEZWA.HAKUNA KITU KAMA HICHO,WAANDISHI WA HABARI MLIO WENGI MNACHANGIA MAOVU.
ReplyDeleteSi kuchangia maovu. Wakuu wa mikoa na wilaya ni ccm. Wasiwtumie makanisa, misimiti kwa manufaa ya chama chao .makanisa na misikiti isikubali kutumika na chama tawala. Badala yake waone ukwrli uliopo. Kama ni waoga nao pia waswapotoshe waumini na wakae pembeni. Waachieni wenye ujasiri waijomboe nchi.wote watu wa dini mko chini ya sheria za nchi ambazo zipo chini ya katiba iliyowejwa uvunguni kwa woga.
ReplyDelete