Bulaya: Nimemsamehe Wassira

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MSUGUANO uliodumu kwa muda mrefu kati ya Esther Amosi Bulaya na Stephen Wassira, umefika kikomo, anaandika Pendo Omary.

Kauli ya Bulaya ambaye ni Mbunge wa Bunda Mjini kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) inaakisi kufungua ukurasa mpya dhidi ya hasimu wake wa kisiasa wa muda mrefu na mwanasiasa mkongwe Stephen Wassira.

“Nimemsamehe Mzee Wassiri,” ni kauli aliyoitoa Bulaya wakati akizungumza na mwandishi wa habari hii leo kuhusu harakati za kisasa jimboni kwake pia hatma ya msuguano kati yake na Wassira uliokuwepo kwa muda mrefu.

Msuguano kati ya Wassira na Bulaya ulianza wakati Bulaya akiwa ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) na muda mfupi baada ya (Bulaya) kuonesha dalili ya kulitaka jimbo hilo lililokuwa likiongozwa na Wassira.

Hata baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka jana, msuguano huo uliendelea na hata Wassira kwenda mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi kutokana na Bulaya kutangazwa mshundi.

“Sikutegemea kama Wassira angenishitaki, nilitarajia angenipa ushirkiano na kunipa uzoefu ili tufanye kazi nzuri ya kuwapatia maendeleo wananchi wa Bunda Mjini,” amesema Bulaya ambapo maelezo zaidi yamo kwenye gazeti la MwanaHALISI la Jumatatu wiki ijayo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Asante dada yangu
    lakini sidhania atakupa ushirikiano wowote labda magu ampe ulaji
    kama kawaida yao ccm

    ReplyDelete

Top Post Ad