AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Ni zaidi ya miezi miwili sasa mkali huyo akiwa kwenye maisha ya ndoa ambapo akichonga na gazeti hili MwanaFA amefunguka mambo matatu ambayo hayafanyi tangu ‘avute jiko.’ Msikie mwenyewe;
Kupiga Misele sana: “Kwa kweli tangu nioe, imenibidi kupunguza baadhi ya ratiba ambazo zilikuwa zinanichukulia ‘time’ huko nyuma na kunifanya wakati mwingine kuwa nje ya nyumbani. Kwa kuwa mimi siyo mtu wa kujirusha kiivo, suala hili limekuwa rahisi na inanipasa kuwa karibu zaidi na familia.
Kuondoa mtazamo hasi juu ya ndoa. “Kipindi cha nyuma nilikuwa ‘sometime’ nasikia kuwa mtu akioa hasa msanii kuna uwezekano mkubwa wa kupotea kwenye gemu, si kweli, mtazamo huo tangu nioe nimeuondoa kabisa kwa kuwa mke wangu ni mtu wa burudani na anafahamu ninachokifanya. Kikubwa ni kupanga ratiba juu ya mambo yangu na kujua nini natakiwa nifanye katika wakati husika.”
Kujisahau. “ Kuna wakati unafika ukiwa mwenyewe tena mwenye mafanikio unaweza kujisahau na kuona kuwa umefika, mafanikio uliyoyapata yanatosha. Lakini ukweli ni kwamba kutokana na kuwa na familia inanibidi kufanya kazi kwa bidii, kwa kuwekeza kwenye muziki wangu na mambo mengine ili kuhakikisha familia yangu inapata kila kitu inachokitaka. Zaidi ni kuwaandalia maisha bora ya leo na kesho!”
Mbali na hayo MwanaFA alimaliza kwa kuwashauri wanamuziki ambao wanayaogopa maisha ya ndoa na kuamini wakifanya hivyo watafeli kuondoa mtazamo huo na kuwahakikishia kuwa familia ni jambo la heri na humfanya mtu kukomaa zaidi ili kufika mbali
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK