AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Rais Magufuli aliyasema hayo jana jioni, katika ziara yake ya kikazi visiwani Pemba. Wakati Rais Magufuli akichaguliwa katika uchaguzi wa Oktoba mwaka jana, Dk. Shein alichaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar kufuatia uchaguzi wa marudio uliofanyika Machi mwaka huu.
“Nampongeza sana Jecha kwa kazi nzuri aliyofanya kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar, na kwa kweli Dk. Shein kama kuna tuzo zako utakazotoa, naomba usimsahau kumpa na Jecha,” alisema Rais Magufuli.
Rai Magufuli pia alimtaka Rais huyo wa Zanzibar kumtaarifu yeye ili awashughulikie watu wote wanaomsumbua visiwani humo au wanaoonekana kumzidi nguvu.
“Rais Shein kama kuna mtu unaona anakusumbua wewe au anakupa tabu nijulishe mimi tu, hata dakika tano hazitapita nitamshughulikia,” ameeleza.
Kauli hiyo inakuja, ikiwa ni zaidi ya miezi kumi sasa tangu hali ya mahusiano baina ya wananchi wa Zanzibar iwe tete, tangu pale Jecha Salim Jecha, Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi visiwani humo (ZEC) alipotangaza kufuta matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka jana.
Mahusiano hayo mabaya yamesababisha, wafuasi wa vyama vya CUF na CCM vyenye nguvu zaidi visiwani humo, kufikia hatua ya kusitisha ushirikiano katika shuguli za kiuchumi na kijamii ikiwemo kutohudhuria misiba na kutonunua bidhaa za mtu wasiyeendana naye kiitikadi.
“Niombe vyombo vya ulinzi na usalama wafuatilie hao wanaokatakata na kuchoma karafuu washughulikiwe bila huruma. Atakayejaribu kuichezea amani, atacheza yeye tena mchezo asiojua kuucheza,” aling’aka Rais Magufuli.
Tangu kufutwa kwa uchaguzi mkuu wa mwaka jana visiwani Zanzibar, hali ya usalama imekuwa si ya kuridhisha.
Nyumba na mashamba ya karafuu yamekuwa yakichomwa moto, huku baadhi ya watu wakitiwa mbaroni na vyombo vya dola kwa tuhuma hizo
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Ujinga mtupu
ReplyDeleteUchwara wote hao
ReplyDeleteNasikia kutapika
ReplyDeleteWametutoka wote wawili
Madikteta uchwara
Fuck fuck fuck
Rais mzima unashabikia wizi wa kura
ReplyDeleteInatutia wasi wasi hata wewe uliiiba kura zetu
Inchi haingozwi kijeshi?
Hata mfanyeje CCM haitakuwa milele Tanzania
Yote haya mtaja yalipa
Mungu awalaani nyote
Kwa uongo na unafiki
akulaani wewe na familia yako yote, peleka maujinga yako kule mfyuuuu
DeleteYa Tanganyika hujayamaliza na una dandandia ya Zanzibar
ReplyDeleteKweli Tindu anasema u kweli u dikteta uchwara na rais mpunga chuya
Inchi inaendeshwa kikatiba magufuli
ReplyDeleteHaiendeshwi kwa utashi au uamuzi wa rais
Inaangilia kichwani kwani upinzani wanakuita dikteta uchwara
Kwa sisi watu wa pwani ni mtu mropkaji
Mbavu
Hajui asemalo
Wala hakujui jinsi ya kuongoza
Hafuati katiba
Mwisho
NI LIMBUKENI WA CHEO