CHADEMA Watoa Onyo: Hatutakubali Tena Kudhulumiwa 2020

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo(Chadema) ,Vincent Mashinji amesema hawatakubali tena kudhulumiwa kwa namna yoyote  katika uchaguzi wa mwaka 2020.

Dk. Mashinji amesema hayo huku akimtolea mfano wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha, na kuongeza kuwa kuna mambo hutokea bila kutarajia lakini watapambana kwa kila hali,

“Huu ni uchaguzi kuna mtu alitarajia haya yaliyofanywa na Jecha? hii inaonyesha kwenye nchi yetu bado kuna tatizo la utendaji haki, wewe umefanya mara ya kwanza tukanyamaza,ukafanya tena mara ya pili kibabe,tukalalamika, badala ya kutuita tuongee, unasema nendeni mkaseme kokote kule”alisema Mashinji.

Aidha, akiongelea utawala wa Rais Magufuli ,Mashinji amesema kumekuwa na ukiukwaji mkubwa wa utawala bora na matokeo yake yeye ndio amekuwa kila kitu, ameongeza kuwa wakati anaanza  mapambano na rushwa aliamini kwamba angeweza kuliondoa tatizo hilo lakini imekuwa tofauti.

Hata hivyo, Mashinji ameongeza kuwa katika mwaka mmoja wa Rais Magufuli, amesema ameshindwa kusimamia utawala bora baada ya kupiga marufuku mikutano ya hadhara pamoja na shughuli zote za kisiasa nchini kwa kile alichosema kuwa muda wa siasa umekwisha.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

3 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Hiyo kama sisi wananchi tutakutakeni. Kwa taarifa zenu wote ni kwamba tumewajua na siasa za matokea hivi sasa they are owned by Jpjm. sera hamna na hatukutakeni tena. Tanzania inabadilishwa kuwa mpya na mwelekeo wa akili zetu pia unafocus Maendeleo ya nchi. nyinyi hata bungeni mnakimbia kutafuta Dili huko nje!!! Tumesha wasoma. tafuteni ustaarabu mwingine na sio siasa

    ReplyDelete
  2. Hiyo kama sisi wananchi tutakutakeni. Kwa taarifa zenu wote ni kwamba tumewajua na siasa za matokea hivi sasa they are owned by Jpjm. sera hamna na hatukutakeni tena. Tanzania inabadilishwa kuwa mpya na mwelekeo wa akili zetu pia unafocus Maendeleo ya nchi. nyinyi hata bungeni mnakimbia kutafuta Dili huko nje!!! Tumesha wasoma. tafuteni ustaarabu mwingine na sio siasa..HAPA KAZI TU

    ReplyDelete
  3. Endeleeni kujitekenya wenyewe

    ReplyDelete

Top Post Ad