AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Kilichotokea: Usiku wa saa tano siku ya Alhamisi (juzi) nilisimamishwa na gari baada kupigiwa honi na kuwashiwa taa na gari iliyokuwa nyuma yangu. Niliposhusha kioo driver akawa anaongea haraka haraka kwamba nimewagonga wakati narudi nyuma parking na nakimbia. Nikamjibu kwamba sijamgonga.
Akaniambia umetugonga angalia bampa. Kweli bampa lilikuwa limelegea. Ila sikuwa nimewagonga hivyo nikaendelea kubisha. Akaniambia shuka uangalie hata pembeni. Alikuwa amevaa smart tu so nikashuka. Wakati naangalia anaposema nimemgonga wakashuka wengine wawili kutoka kwenye gari na kunishika. Wakaanza kunishambulia huku wakinipora wallet, saa nk. Then wakanikata panga kichwani na kupekua gari wakaondoka na laptop na simu pamoja na funguo wa gari.
Kwa sasa naendelea vizuri baada ya kupata matibabu. Nawashukuru wote.
Albert Msando
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Pole sana kaka mungu aendelee kukutetea
ReplyDeletePole sana,hii inafanana na yaliyonitokea wiki mbili zilizopita ila mimi chale zilinicheza,sikujali nini wanasema wala kushuka kwenye gari bali niliwaambia nifuateni nyuma twende polisi,na bila shaka hao umetoka nao mbali bila wewe kujua,wana mtandao wao.Ni aina mojawapo ya mbinu za uporaji,wao ndio wamelegeza bampa au wanagonga taa yako hata wanakugonga au kuvunja chochote ili mradi tu uingie kwenye mtego,na mara nyingi wanavizia sehemu ambayo watu hawako makini kwa tukio lolote,na ukishuka tu wanakushambulia,hivyo hata kama gari lako limegongwa achana nao,bora uende/ujipeleke polisi mwenyewe.
ReplyDeleteMWANDISHI UNATUSHTUA NA UDAKU WAKO,ANDIKA VIZURI.AMEKATWAKATWA AU AMEKATWA?
ReplyDelete