AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
KIMUHEMUHE kilitanda kwenye viunga vya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Feb 17, 2017, kufuatia ndugu, jamaa na marafiki wa model, Agness Masogange kufurika huku wakitarajia kumuona ndugu yao huyo akifikishwa mahakamani hapo .
Ndugu hao waliwasili Kisutu mapema asubuhi na kuweka kambi mahakami ili kusikiliza kesi ya masogange anayehusishwa na tuhuma za matumizi ya dawa za kuleya.
Licha ya Masogange kutokufikishwa mahakamani hapo kwa kile kinachodaiwa kuwa majibu ya Mkemia Mkuu wa Serikali kuhusu kipimo endapo mwanadada huyo anatumia madawa ya kulevya, kilikuwa hakijatoka lakini mpaka ilipotimu majira ya saa 9:00 mchana, ndugu hao walikuwa hawajakata tamaa. Baada ya kuona hakuna dalili zozote kwa ndugu yao kuletwa mahakamani hapo huku muda wa mahakama wa saa 9:30 ukiisha, ndipo ndugu hao waliamua kuondoka kwa unyonge eneo la Kisutu.
Taarifa iliyotolewa jana na Kamnada wa Polisi Kanda Maalum ya Dar, Kamishna Somon Sirro ilieleza kuwa, Masogange na wenzake 17, wanashikiliwa na jeshi hilo kwa tuhuma za kuhusika na matumizi ya dawa za kulevya, na kwamba jana walipelekwa kwa Mkemia Mkuu wa Serkali kwa ajili ya vipimo na endapo ikibainika wanatumia madawa ya kulevya, leo Ijumaa au Jumatatu ijayo watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK