Dodoma: Wanywaji wa Pombe za Viroba Waja na Mbinu Mpya..!!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Baada ya sekeseke la kupiga marufuku uuzaji na unywaji wa pombe kali viroba, wanywaji wa pombe za viroba mjini Dodoma wamebuni mbinu mpya ya kununua pombe hiyo iliyopigwa marufuku huku watumiaji hao wakiipa pombe hiyo jina la maziwa mgando au nzela.

Maeneo yanakopatikana viroba kwa wingi katika mji huo ni stendi ya Mkoa wa Dodoma na Jamatini ambapo wafanyabiashara humimina pombe hiyo katika chupa za konyagi.

Uchunguzi uliofanywa na gazeti la Mtanzania kwa siku kadhaa mjini hapo, umeonyesha jinsi pombe hiyo inavyouzwa kwa shilingi 1,000 baada ya kujazwa kwenye chupa kubwa za konyagi.

Mmoja wa wauzaji wa pombe hiyo ambaye hakutaka kuandikwa jina lake gazetini, alisema biashara imekuwa ngumu na wao wanahitaji kupata fedha, hivyo wameamua kuja na njia mpya ya kuuza viroba hivyo. “Tutafanyaje ndugu yangu, maisha magumu, tumeweka viroba katika chupa kubwa za konyagi na tunawapimia kwa kutumia kakikombe kadogo kama ka kahawa kwa shilingi 1,000,” alisema mfanyabiashara huyo.

Aliongeza”Siwezi kuacha hii biashara, hapa ni stendi, wasafiri na makondakta wengi ndio wateja wetu na natengeneza fedha za kutosha, lakini sasa hivi nawauzia tu watu ninaowajua, kwani naogopa kukamatwa.”

Naye mmoja wa wanunuzi wa viroba hivyo, alisema baada ya Serikali kupiga marufuku uuzwaji wa viroba hivyo, wameamua kubadili mwelekeo wa kununua bidhaa hiyo ili kukwepa mkono wa Serikali.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad