Duh..Huyu Harmorapa Huyu..Eti Amesema Hii Ndiyo Sababu ya Kumpigia Magoti Ali Kiba....!!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Msanii wa muziki wa hip hop, Harmorapa amefunguka kwa kudai kuwa Tanzania hajaona msanii wa kumfananisha na Alikiba na kusema hata ngoma yake ambayo amefanya na Juma Nature alitaka kufanya na Alikiba.

Rapper huyo alikuwa mmoja kati ya watu waliojitokeza JK Nyerere Airport kumpokea muimbaji huyo wa wimbo Aje kitokea Afrika Kusini.

Katika tukio hilo rapper huyo alionekana akipigia magoti muimbaji huyo huku akimkabidhi tisheti tukio ambalo lilizua maswali mengi.

Akiongea katika kipindi cha Enewz cha EATV, Harmorapa alidai yeye anamkubali sana Alikiba ndio maana akafanya kitendo hicho.

“Kiukweli King Kiba kwa Tanzania hapa sioni wa kumfananisha naye, kwa hiyo nisema sijaona bado wa kumlinganisha naye sababu jamaa anafanya vizuri sana na anajua muziki sana, hata kabla ya kurekodi hii kazi yangu mpya nilifanya jitihada na watu wa karibu na Alikiba japo niweze kufanya naye kazi lakini sikuweza kufanikiwa kutokana na mambo yake kuwa mengi sana na watu pia ambao walikuwa wakinipa connection naye kuna vitu sikuweka sawa, na muda nikaona unazidi kwenda nikasema ngoja nifanye tu” alisema Harmorapa

Aliongeza, “Hata ishu ya kumpigia magoti ni kuonyesha kwamba namkubali, ni heshima kwake, sidhani kama kuna tatizo hapo,”

Rapper huyo hivi karibuni ameachia wimbo wake mpya ‘Kiboko ya Mabishoo’ akiwa amemshirikisha Juma Nature.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. kumpigia magoti ni ujinga hata kama unamkubali na unajidhalilisha

    ReplyDelete

Top Post Ad