AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki Dar es Salaam muhadhama Askofu Kardinal Polcarp Pengo, ametunukiwa cheti na Umoja wa Wanaume Wakatoliiki (Uwaka ) kwa kupanda Mlima Kilimanjaro.
Alikabidhiwa cheti hicho jana na Msaidizi wa Jimbo hilo Mhashamu Eusebius Nzigilwa.
Askofu Pengo hata hivyo alieleza kuwa hakufanikiwa kufika kwenye kilele cha mlima huo isipokuwa alithubutu pamoja na waumini wengine kadhaa, ambapo wachache miongoni mwao ndiyo walifanikiwa.
"Naamini kwamba hao wachache walifanikiwa kufika kwenye kilele cha Mlima Kilimanjaro kwa sababu sisi tulianza nao hivyo walipata moyo, haitakiwi mwanaume uwe na moyo wa kukata tamaa," alisema Askofu Pengo huku akiwa amekaa kwenye kiti.
Pengo aliyasema hayo kwenye ibada ya maadhimisho ya Uwaka wakisheherekea msimamizi wao Mtakatifu Yosefu na Jubilei ya miaka 100 ya Upadre Tanzania.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK