Inatosha...!!! Harmorapa Atoa Povu kwa Wanaomsema Vibaya Kuhusu Sura Yake na Mziki Wake...!!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Rapper ambaye kwa sasa ana kiki kubwa Bongo, Harmorapa amezungumzia madai kwamba anabebwa na wimbi la kiki wala hayupo kwenye game kudumu.

Hakijatosha, Harmorapa alipata nafasi pia kuzungumzia ishu ya wanaomuongelea vibaya na hata kumtukana. Nilipata nafasi ya kupiga stori na Harmo na alikuwa na la kuwaambia wanaomsema vibaya. “Watu ambao wanahisi Harmorapa hatodumu kwenye game kwanza wanakosea halafu pia naweza nikasema kwamba wanamkufuru Mungu kwa sababu Mungu ndiye anayepanga na kupangua,” alisema rapper huyo.

Aliendelea kusema…”Kama mimi binafsi nimejipanga sana vya kutosha. Unajua kwamba maneno yao mimi hayanivinjii chochote ni ile sawa na kumpiga chura teke na kumwongezea mwendo. Wanavyoniongea mimi ndo wananipa power na wananipa maujuzi na wananipa kuweza. Ni wao wananiweza mimi kuweza na kukaza ilmradi niweze kufanya kazi nzuri.”

Katika hatua nyingine nilitaka kujua iwapo Harmonize amemjua kabla awe supa staa au vipi. Alinijibu kwa kusema kwamba hakuwa akimfahamu muimbaji huyo kutoka WCB kabla hajakuwa staa. Wakati akiendelea kufanya vizuri na wimbo wake wa ‘Kiboko ya Mabishoo’, Harmorapa amewaahidi mashabiki wake makubwa mwaka huu na amewataka wawe tayari kushuhudia maangamizi atakayofanya kwenye game mwaka huu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad