Ishara Kumi Kwamba Wewe ni “Mwanaume Suruali” Mbele ya Wanawake!...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Hakuna mwanaume asiyependa kuonekana yeye ni mwanaume bora, rijali na anaekubalika mbele ya jamii. Lakini mara nyingi tunapojaribu kufanya kila tuwezalo ili tuwe wanaume bora,mara nyingine tumejikuta Tunaharibu zaidi na kuonekana “wanaume suruali”, “nice guy” na majina mengi yakiwa na maana ya mwanaume mdhaifu, na asiye na sauti mbele ya wanawake au mpenzi wake.

Ukiona una ishara hizi, Tafuta namna ya Kubadilika.

a) Huna Mpenzi na una marafiki wengi sana wa kike. Na wamekuwa wakikuelezea matatizo ya wapenzi wao, na wewe unajiona ni mshauri wao bora!



b) Kama una mpenzi, Unakubaliana na kila anachokisema au anachokitaka unasahau kuwa, wakati mwingine wanawake hufanya vitu kwa majaribio kuona utakubali? Na ukikubali, basi ushakuwa “uchochoro” atakulazimisha ufanye kila anachokitaka kwa gia ya “mimi si ni mpenzi/mke wako??”

c) Huna muda na Marafiki zako tena! Wakati mwingine unakataa mialiko yao kutokana na Pengine mpenzi wako kakuomba umsindikize rafiki yake shopping, au saluni

d) Una rafiki mwanamke ambae si mpenzi wako, unamjua mpenzi wake, lakini wewe ndo unaongea nae zaidi kwenye simu (hasa usiku) kuliko mpenzi wake, wakiwa pamoja wewe ni mpiga picha wao (cameraman) na kuwanunulia maji nk.

e) Unapenda sana kioo kuliko vitu vingine! Na mara nyingi unajipiga picha mbele ya kioo

f) Ni mtu wa Kujitolea mno hasa kwenye kazi ambazo hakuna anayependa kuzifanya. kama kuwabebea wengine mizigo mnapotembea nk!

g) Siku zote wewe ni mtu unayeweka maslahi ya watu wengine mbele kabla yako. Unatumwa mno na mtu yeyote na Hujui Kusema hapana

h) Mpenzi wako ndiye mwenye maamuzi ya mwisho “mi nakusikiliza wewe!”

i) Baada ya party, siku zote wewe ni mstari wa mbele kusafisha meza pamoja na wanawake! Na wanawake wanakupenda kwa hilo.


k) Mkitoka “out” , mpenzi wako analeta marafiki zake kibao na unawalipia pia
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad