Jokate Akerwa na Matusi kwa Wanawake...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanamitindo maarufu nchini, Jokate Mwegelo amewataka watu kuacha kutumia lugha za maneno makali (matusi) dhidi ya wanawake kwa kuwa wanawake ni watu wanaohifadhi maumivu na mambo mengi  kwenye moyo zaidi ya wanaume.

Jana wakati akikabidhi mchango wake EATV katika kampeni ya 'Namthamini', Jokate amesema mwanamke ni mtu ambaye anakumbana na mambo makubwa anayopaswa kukabiliana nayo mengine ni mazito lakini anayaweka moyoni mwake ili kufanikisha jambo hivyo anapaswa kuheshimiwa.

"Najisikia vibaya sana pale ambapo mtu namsikia anatoa lugha ya matusi kwa mwanamke, Wanawake tunaumia zaidi ya mara 1000 kwa mwanamke, mwanamke anahifadhi mambo mengi sana moyoni kitu ambacho hakitakiwi, wanawake wanapaswa kuheshimiwa na kulelewa katika jamii na wanastahili kuthaminiwa". Amesema Jokate

Ameongeza kuwa yeye kwa upande wake mwanamke ni mtu mwenye moyo wa ziada ambaye hujitoa kwa ajili ya jamii lakini pia ni mchapa kazi na anajua kitu gani anataka.

Katika kampeni ya Namthamini inayoendeshwa na EATV kuwachangia mabinti waende shule bila kukosa kwa kigezo cha kuepuka aibu inayosababishwa na ukosefu wa vifaa vya kujisitiri kipindi cha hedhi, Jokate amechangia kiasi cha shilingi laki moja.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad