Kama Ulimiss Jinsi Ruge Alivyofunguka Kuhusu Paul Makonda Basi Nimekuwekea Video Hapa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Ruge: Niliwambia SHILAWADU siku ya Alhamisi mchana kuwa wasiirushe 'Story' bila kuongea na upande wa pili (wa Gwajima)

Ruge: Niliwambia Vijana wa SHILAWADU kuwa 'Story' kama ndo anayoisubiri RC basi ajue haitaenda hewani hata kwny Social Media

Ruge: Ijumaa niliwasisitiza SHILAWADU kuwa kipindi kile kisirushwe kwakuwa 'Story' haiko balanced

Ruge: Ijumaa saa 5 kasoro usiku nilipigiwa simu kuwa RC Makonda alikuwa kaja ofisini akiwa na maaskari wakiwa na silaha

Ruge: Nilimpigia simu RC Makonda kumhoji kwanini aje ofisini na maaskari wenye silaha? Akauliza kwanini nimezuia kipindi kuruka!?

Ruge: RC Makonda alikata simu, lkn nilipaniki nikiwazia hizo silaha walizokuja nazo ofisini. Makonda alikichukua kipindi kwny flash

Ruge: RC Makonda alisema "Bahati yenu" baada ya kujua kuwa waliokataa vijana wa SHILAWADU sio waliozuia kipindi isipokuwa mimi

Ruge: Nilimwambia Mkurugenzi wa Clouds(Kusaga) kuwa RC alitukosea heshima; kulikuwa na haja gani aje na silaha na ni rafiki yetu?

Ruge: Ukweli hakuna aliyepigwa ila kulijengwa hofu kubwa kwa wafanyakazi wa Clouds Media. Si jambo dogo hili!

Ruge: Tusikwepe ukweli kuwa sisi Clouds Media kama chombo cha habari tuna wajibu wa ku-balance story. Sijawahi kulazimishwa story...

Ruge: Kuacha shughuli za kazi, Makonda amekuwa akija hapa Clouds kama rafiki. Ila kitendo cha kuja na walinzi kiliwashtua walinzi

Ruge: Kama watanzania, hatutaki kuiona bunduki mitaani. Hili limetokea kutufungua macho kujua ma-RC na ma-DC wanavyofanya kazi yao...

Ruge: Sisi tuhukumiwe kama taasisi, wafanyakazi wetu wasitiwe hofu. Mimi sikuwekwa ndani, nilienda Polisi kuripoti suala hili

Ruge: Mtu akikosea kabla hatujaangalia cheo chake, tuangalie makosa yake. Si kudai eti wanaomkosoa wanapingana Vita ya #DawaZaKulevya

Ruge: Mtu kuwa na nafasi ya Uongozi flani si sababu ya 'kuwapanda' watu . All we want is RESPECT!

Ruge: Video clips za CCTV zinazozunguka mtandaoni kweli ni za hapa Clouds Media. Sisi tulidhani Makonda angeomba radhi kwa kadhia hii

Ruge: Siujutii ukaribu wangu na Makonda. Hata akirudi akaomba radhi bado nitamfikiria! Tunataka kuendelea kumpa ushirikiano

Ruge: Niseme, urafiki na BUNDUKI siutaki. Wanaodai Makonda alikuja hapa Clouds akiwa rafiki wanapotosha! Ametumia vibaya madaraka

Ruge: Clouds inalaani kilichotokea, na inaomba Vyombo vya Habari vitoe ushirikiano ktk kukemea hili. Hatutaki kugombana na Serikali

 Tazama Video:


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. that is not fare at all Raisi Magufuli mbona unatuangusha anae kosa lazima apewe adhabu huyumakobda sijui daudi sijui bashite vp akucheze akili yako hivo mbona mkuu wa mkoa anavuka mipaka yake kweli unajua kusoma kunachangia sasa ni 100% imedhihirisha jamaa ni zero kweli this is a big shame

    ReplyDelete
  2. kwani si ni walinzi wake tu,mbona picha zinaonyesha amani tu na hakuna mtu amekabwa na polisi au mbona hatuoni kama kuna kujibishana vibaya?Lazima muungane wengi katika nyie hamtaki dawa za kulevya zipingwe,mbona mwajulikana.

    ReplyDelete

Top Post Ad