Kigogo ALAT Atumbuliwa Hadharani kwa 'Kupiga' Mil 90...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwenyekiti wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa nchini ALAT Bwana Gulam Mukadam amemsimamisha kazi Katibu Mtendaji wa Jumuiya hiyo Bw Abraham Shemoboyo kupisha uchunguzi wa tuhuma za ubadhirifu wa shilingi milioni 150 za ufadhili wa jumuiya hiyo mwaka 2015.

Akiongea  katika ofisi za jumuiya hiyo Jijini Dar es salaam, Gulam ambaye pia ni Mstahiki Meya wa Manispaa ya Shinyanga amesema, benki ya NMB ilitoa kiasi hicho cha pesa kwa jumuiya hiyo kwaajili ya ufadhili wa Tuzo ya Meya (Mayor Awards) na kwamba Katibu huyo huyo hakuwasilisha kiasi chote na badala yake aliwasilisha shilingi milioni 60 huku kiasi cha shilingi milioni 90 kikiwa hakijulikani kilipo.

Mukadam amesema, uamuzi wa kumsimamisha uliamuliwa na kamati tendaji ya ALAT Taifa na mkutano mkuu wa ALAT taifa, ambapo iliundwa tume ndogo kuchunguza upotevu wa kiasi hicho cha pesa na kuamuliwa kuwa apishe uchunguzi dhidi yake kwa upotevu wa pesa hizo.

Aidha Mstahiki Mukadam amesema, uchunguzi dhidi yake utafanywa na CAG na kwamba pesa hizo hazikuwekwa kwenye akaunt ya ALAT na badala yake zilihifadhiwa kwenye akaunti binafsi ijulikanayo kama 'Vision Investment'.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad