Usafi kwa Wanaume: Namna Nzuri ya Kutunza Uume...!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mgegedo ni tafsida nimeitumia kama kiwakilishi cha maumbile ya mwanaume yaani uume. Mgegedo ni eneo muhimu sana kwawanaume ambalo wanalitukuza kuliko kitu chochote hapa duniani, hivyo leo hiinimeona ni vyema kutoa darasa kwa wanaume ili wajue namna nzuri ya kutunza migegedoyao ili iwe misafi na yenye afya kwa ustawa wa mahusiano yao na wenzi wao.

Ni vyema wanaume wakajengautaratibu wa kuweka migegedo yao katika hali ya usafi unaostahili kwa ajili yakujenga mahusiano mazuri na wenzi wao inashauriwa kuosha mgegedo kwamakini kwa kutumia maji ya uvuguvugu kila siku mwanaume anapooga, kama mwanaumeatakuwa hajatahiriwa, basi anatakiwa kuigeuza ile ngozi inayofunika sehemu yambele ya mgegedo wake na kuisafisha kwa makini ili kuondoa ukando kando unaokuwaumeganda ndani unaofanana na jibini ambapo ukando kando huo hufahamikakitaalamu kama smegma.

Huu ukando kando unaopatikanandani ya migegedo ya wanaume wasiotahiriwa ni kilainishi maalum kinachoufanyamgegedo usiwe mkavu,kilainishi hiki ni cha kimaumbile.

Kama kilainishi hiki kikiachwabila kusafishwa kwa muda mrefu kitaanza kutoa harufu mbaya na baadayekitazalisha vijidudu (bacteria) ambavyo vitasababisha mgegedo kuvimba na kuwamwekundu sehemu ya mbele ambapo tatizo hilo hufahamika kitaamu kama balanitis.

Mwanaume asiyetahiriwa asiyesafishamgegedo wake vizuri licha ya kupatamatatizo niliyoyaeleza hapo juu lakini pia huweza kuharibu mahusiano yake namwenzi wake. Hakuna mwanamke ambaye atapenda kujinafasi kwa kulamba koni yamgegedo usio msafi, kwani ni kujitafutia fangasi za kinywa.

Hata hivyo ningependa kuwaonya kina mama kamwe wasijaribu kuigeuza ngozi ya migegedo ya watoto wao wadogo ambao hawajatahiriwa, kwani hiyo inaweza kuwaumiza na kuwasababishia maumivu makali. Kwa kawaida ngozi ya mbele ya migegegdo ya watoto wadogo inakuwaimeshikana na kichwa cha mgegedo hivyo haiwezi kuvutika yote na ukilazimisha unaweza kumjeruhi. Kwa watoto wadogo katika makuzi yao hawahitaji kusafishwa migegedo yao kwa namna hiyo. 

Lakini pia pamoja nakwamba usafi ni muhimu lakini haishauriwi kusafisha migegedo kwa kiwangokilichopitiliza kwa kutumia sabuni ya kipande au ya maji kunaweza kusababisha muwasho na uvimbe kwenye mgegedo hususani kwa wanaume wasiotahiriwa.Kwa kusafisha mgegedo mara mojakwa siku kwa maji ya uvuguvugu inasaidia kuiweka migegedo katika hali ya usafi kiafya. Na kama unataka kutumia sabuni, ni nyema kutumia sabuni zisizo za manukato yaani wengine huita sabuni mbuni au sabuni ya kipande. Kwa kutumia sabuni za manukato unaweza kusababisha muwasho na uvimbe wa ngozi wa mgegedo wako.

Usafi wa eneo la korodani za mgegedo

Kuzungumzia usafi wa mgegedo sikwamba nimesahau kuzungumzia usafi wasehemu ya chini ya mgegedo yaani korodani. Eneo la korodani lisipofanyiwa usafi makini lile jasho na nywele za chini husababisha harufu Fulani yenye kukera. Eeneo la korodani linatakiwa kufanyiwa usafi makini hasa kwa wale wanaovaa nguo za ndani muda wote kwa siku nzima. Ni vyema kuhakikisha eneo lachini la korodani karibu na sehemu ya kutolea haja kubwa inakuwa safi wakatiwote ili isiwe na harufu isiyovutia.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad