BAADA ya Tetesi Kuwa Nyingi juu ya Dogo Asley Kutaka Kujieungua na Ya Moto Band..Said Fella Ameibuka na Haya..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mkurugenzi wa Yamoto Band, Saidi Fella ‘Mkubwa Fella’ amedai kuwa hakuna msanii aliyekatazwa kuondoka ndani kundi hilo.

Aidha amedai kuwa wasanii wa bendi hiyo wanaruhusiwa kufanya project zao binafsi za muziki.

Fella ambaye ni mlezi wa wasanii 106, amesema kuwa kituo chake ni kama shule, yeyote ambae anajiona amekuwa anaweza kuondoka.

“Hakuna msanii ambaye amekatazwa kuondoka Yamoto Band hata Mkubwa na Wanawe ila ukiondoka bila kuaga haufiki sehemu yoyote,” alisema Fella.

Aliongeza, “Mimi nawasaidia kuwaonyesha njia wafike sehemu fulani, mtu akijiona amekuwa kwanini nimzuie?. Hakuna aliyefungwa kwa namna yoyote, sema ni vyema mtu kufuata taratibu hata za makuliano yetu ya mdomo,”

Pia Fella alidai hakuna msanii aliyekatazwa kuachia kazi zake binafsi.

“Aslay hivi karibuni ameachia kazi yake mpya na sisi tunamsupport kwa sababu kabla ya Yamoto Band, Aslay alikuwa msanii ila sisi tulimtumia yeye kuwainua wenzake na kweli tumefanikiwa leo hii vijana wanapata makate wao wa kila siku. Kwa hiyo hata wasanii wenzake wanaweza kufanya hivyo pia lakini kama wanamakubaliano yao binafsi siwezi kuyaingilia,” alisema Fella.

Bendi hiyo kwa sasa inafanya vizuri na wimbo ‘Basi’
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad