CAG Afichua Ufisadi Mkubwa Serikalini..Aeleza Jinsi Misamaha ya Kodi Inavyoitafuna Nchi..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Prof. Mussa Assad, imebaini kuwapo kwa matumizi mabaya ya msamaha wa kodi wa shilingi bilioni 3.46, uliotolewa kwa walengwa wawili walioagiza jumla ya magari 238 mwaka wa fedha wa 2015/16.

Akiwasilisha ripoti ya matokeo ya ukaguzi kwa mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2016 katika mkutano wa saba na kikao cha saba cha Bunge, Prof. Assad amesema, msamaha huo wa kodi ulitolewa, lakini magari hayo yalisajiliwa kwa majina ya watu tofauti na wale waliopewa msamaha.

Hata hivyo, amesema walengwa wote waliopewa msahaa huo walikana kuhusika na magari hayo, hali inayoonyesha bado kuna uhitaji wa kuboresha udhibiti na ufuatiliaji wa masuala ya misamaha ya kodi.

Katika udhibiti wa misahaha ya mafuta yanayoingizwa nchini kwa ajili ya matumizi ya migodi, Prof. Assad amesema katika ukaguzi walioufanya Mei 31, mwaka jana, wamebaini lita za mafuta 4,248,802 yaliyosafirishwa kutoka jijini Dar es salaam kati ya Oktoba 2014 na Disemba 2015 kwa ajili ya matumizi ya mgodi wa Buzwagi, Bulyankulu na Geita, nyaraka za uthibitisho hazikuweza kufika vituo husika na kuonesha mafuta hayo yaliyosamehewa kodi yalitumika tofauti na makusudi.

Pia hiyo imebaini lita 20,791,072 za mafuta yenye msamaha wa kodi wa shilingi bilioni 10.17 kwa ajili ya mgodi wa Buzwagi katika kipindi cha miezi 18 kuanzia Julai 2014 hadi Disemba 2015, yalisafirishwa kwenda kampuni ya M/S Agreeko mkandarasi msaidizi ambaye hakuwa mhusika wa msamaha huo.

Kutokana na matumizi hayo mabaya ya msamaha wa kodi, Prof. Assad ameishauri Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kufanya uchunguzi wa mafuta yote ambayo hayana ushahidi kama yamesafirishwa vituo vya uchimbaji madini na kukusanya kodi inayodaiwa kiasi cha shilingi bilioni 1.599 na kodi ya shilingi bilioni 10.17 iliyosamehewa na kupelekwa kwa wakandarasi wasiohusika na msamaha huo.

Aidha, amesema serikali inatakiwa kuhakikisha usimamizi unaimarishwa juu ya matumizi ya misamaha inayotolewa kwa mujibu wa sheria ili kuepuka hasara kwa serikali kutokana na matumizi mabaya ya misamaha ya kodi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad