Hataree..Mzee Mwinyi Afunguka Mazito Kuhusu Tanzania ya Magufuli..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


RAIS mstaafu wa Awamu ya Pili, Ally Hassan Mwinyi amemuomba kiongozi wa dini ya Wahindu ya Swaminarayan Duniani, Mahant Swami Maharaji kuiombea Tanzania amani na umoja viweze kudumu na kusiwepo aina yoyote ya ubaguzi kwa sasa na hata vizazi vijavyo.

Mwinyi aliyasema hayo Dar es Salaam baada ya kualikwa katika hafla ya kumkaribisha kiongozi huyo hapa nchini na kukutana na waumini wa dini hiyo.

Pia ilikua ni maadhimisho ya miaka 40 tangu kujengwa misikiti miwili ya dini hiyo hapa nchini.

Alishukuru kwa kualikwa katika hafla hiyo ya kidini kwani sio jambo la kawaida kupokea ugeni wa kiongozi wa kidini nchini.

“Sina shaka kuwa sio nchi zote wenye kuwa na uwezo wa kumuona kiongozi mwenye nafasi kubwa kama hiyo katika nchi zote,” alisema na kuongeza kuwa kama Watanzania wengine amekuwa mwenye bahati.

Alimkaribisha kiongozi huyo nchini na kumtaka kuiombea sana Tanzania ili iendelee kudumisha amani na umoja na licha ya kutokuwepo kwa aina yoyote ya ubaguzi, aendelee kuomba ili hali hiyo isiwepo kamwe na wananchi waendelee kuishi kama ndugu.

Kwa upande wake, kiongozi huyo ambaye ni wa sita kwa nafasi hiyo, Maharaji alisema ataendelea kuiombea Tanzania na dunia nzima kwa ujumla ili wananchi wake waendelee kubarikiwa katika maisha yao pamoja na kukuza maendeleo yao.

Alisema mwanadamu siku zote hupenda raha lakini ni vyema wakafahamu kuwa hakuna raha kubwa kama kupata kutoka kwa Mungu kwa kuwa raha nyingine zote ni za muda, hazidumu.

“ Starehe ya mwanadamu ni ya muda mfupi na raha ya kuishi anayeitoa ni Mungu na ambayo haidumu, hivyo siku zote yapasa kuomba sana kwa Mungu kupata raha ya kudumu,” alisema na kusisitiza wajibu wa kila mwanadamu kuomba amani siku zote na kila wakati na kuishi kwa kanuni za Mungu.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad