JPM - Ole Wake Atakayeingilia Kamati Niliyoiunda,....!!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli ametoa onyo kali kwa mtu yeyote atakae kwamisha Kamati maalumu aliyoiunda ya  kuchunguza kiwango cha madini yaliyomo kwenye mchanga uliowekwa kwenye makontena.

Amesema kuwa ameamua kuunda kamati hiyo yenye wasomi waliobobea katika masuala ya jiolojia, kemikali na uchambuzi wa kisayansi ili wawakilishe Watanzania zaidi ya milioni hamsini ambao wanataka kujua ukweli kuhusu rasilimali yao ya madini.

“Nendeni popote mnapohitaji kufanya kazi tutawapa ushirikiano, fungueni makontena popote yalipo, chukuenki sampuli mkazipime mjue kilichomo na naviagiza vyombo vya dola vihakikishe hakuna anaekwamisha,”amesema Rais Dkt. Magufuli.

Aidha, pamoja na kuunda kamati hiyo, Rais Magufuli amesema kuwa ataunda kamati nyingine ya wachumi na wanasheria kwa ajili ya kufanya tathmini na kuangalia sera na sheria ya madini kwa lengo la kupata taarifa zaidi juu ya biashara ya madini hapa nchini.

Hata hivyo, ameihakikishia kamati hiyo kutoa ushirikiano mkubwa kutoka Serikalini ili kufanikisha kazi hiyo na amewataka wawe huru kutumia vitendea kazi wanavyohitaji zikiwemo maabara mbali mbali za taasisi za Serikali na nyinginezo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad