AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Msanii mkongwe nchini Tanzania, Juma Nature maarufu kama 'Kiroboto' amefunguka na kusema hajawahi kugombana na msanii mwenzake Chege Chigunda kama watu wanavyofikiri kuwa mwanamke ndiyo amewafanya washindwe hata kusalimiana wawili hao.
Nature amebainisha hayo baada ya kuenea tetesi za kipindi kirefu zilikuwa zinawaaminisha watu kuwa mke aliyemuoa msanii huyo ndiye alikuwa mpenzi wa Chege hapo awali mpaka kupelekea kuimba wimbo wenye maudhui ya kumuaga mpenzi huyo uliyopewa jina la 'Good bye'.
"Mimi sijawahi kugombana na mwanangu, sasa mimi nigombane na damu itawezekana kweli ?, hatuwezi kugombana, tutagombana stejini tu kwa sababu ya usanii lakini hatugombani kama hivyo unavyochukulia wewe". Alisema Juma Nature pindi alipokuwa anazungumza katika kipindi cha eNewz ya EATV
Kwa upande mwingine msanii huyo amesema kwa sasa ameachana na mke wake kwa takribani miaka 7 huku akisisitiza kuwa bado wanaelewana vizuri na hawana ugomvi wowote japokuwa hawapo pamoja tena.
Mtazame hapa kwenye show ya eNewz
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK