AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Tanzania na timu ya KR Genk ya Ubelgiji, Mbwana Samatta, amesema anaamini timu hiyo itaibuka na ushindi nyumbani katika mchezo wa marudiano dhidi ya Celta Vigo na kufuzu nusu fainali ya michuano ya Europa.
Genk ilitandikwa mabao 3-2 ugenini na Celte de Vigo ya Hispania katika mchezo wa kwanza wa michuano hiyo, hivyo inahitaji ushindi katika mchezo wa marudiano ili kufuzu hatua ya nusu fainali.
Akizungumza jana, Samatta alisema wamefanyia kazi kasoro zilizojitokeza kwenye mchezo wa kwanza na kusababisha wapoteze ikiwemo kupoteza nafasi nyingi za wazi, hivyo wana matumaini ya kupata matokeo mazuri katika mchezo wa marudiano.
Alisema anafahamu mechi ya marudiano itakuwa ya ushindani mkubwa, lakini watalazimika kupambana kufa kupona ili waweze kushinda kwenye uwanja wao wa nyumbani.
“Tuna matumaini makubwa ya kufanya vizuri katika mchezo wetu wa marudiano, hivyo tayari benchi la ufundi limeanza kufanyia kazi kasoro zilizojitokeza kwenye mchezo wa kwanza ili zisijirudie tena,” alisema Samatta.
Samatta kwa siku za karibuni amekuwa tegemeo katika kikosi cha KRC Genk aliyojiunganayo akitokea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) aliyoichezea kwa mafanikio makubwa ikiwemo kutwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK