Shahidi Afunguka Mapya Kuhusu Scorpion Mtoboa Macho..Wengi Wapigwa na Butwaa Mahakamani..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


SHAHIDI katika kesi inayomkabili mshitakiwa Salum Njwete ‘Scorpion’, ya kuiba kujeruhi  na  kumtoboa macho Saidi Mrisho amedai mshitakiwa huyo ni mlinzi wa amani.

Katika kesi hiyo iliyoendelea kusikilizwa jana kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, shahidi huyo, Deus Magosa alidai anamfahamu hivyo mshitakiwa.  

Shahidi huyo mkazi wa Buguruni ambaye ni kiongozi wa ulinzi shirikishi wa eneo hilo, alidai kuwa yeye ndiye aliyempa ajira ya ulinzi wa amani mshitakiwa kwenye eneo hilo la biashara ndogondogo.

Mwendesha mashitaka wa Serikali, Nassoro Katuga alimhoji shahidi huyo namna anavyomfahamu Scorpion ambapo mbele ya Hakimu Flora Haule, Magosa (46) alijibu anamfahamu kwani mshitakiwa aliajiriwa na wafanyabiashara wadogo kuwalinda pamoja na biashara zao pamoja na uongozi wao wa ulinzi ushirikishi.

Aliendelea kudai kuwa Salum alikuwa akilipwa Sh 10,000 kwa siku na wafanyabiashara hao kwa kuwawezesha kuendelea na biashara zao bila matukio ya wizi.

Hata hivyo, shahidi huyo alipoulizwa kama anakumbuka kilichotokea Septemba 6 mwaka jana, Magosa alijibu kwamba siku hiyo hakuwapo alikuwa msibani nje ya Dar es Salaam

Aliendelea kudai kuwa aliporudi alisikia watu wakizungumza mtaani, kwamba kuna mtu alitobolewa macho na kujeruhiwa katika tukio lililotokea maeneo ya Buguruni ambapo walimtaja mshitakiwa kuwa ndiye aliyehusika na tukio hilo.

Wakili alimwuliza baada ya hapo nini kiliendelea shahidi akajibu waliitwa Polisi na alipokwenda aliulizwa kama anamfahamu Salum Njwete ambapo alijibu anamfahamu na kumtaka akamwite.

Shahidi alidai alimfuata mshitakiwa na bila shaka wala kukataa alisema yeye ni raia mwema na alikwenda polisi bila kukamatwa na akaambiwa niondoke akamwacha mshitakiwa Polisi Buguruni.

Wakili Katuga alisema kesi hiyo itaendelea kusikilizwa Aprili 18   ushahidi utakapoendelea kutolewa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad