Simba Yaingia Fainali, Yaiadhibu Azam 1 - 0 Kombe la Shirikisho

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


SIMBA SC imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), linalojulikana kama Azam Sports federation Cup baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Azam FC jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 

Sifa zimuendee mfungaji wa bao hilo pekee dakika ya 48, Mohammed ‘Mo’ Ibrahim ambaye hata hivyo hakumaliza mchezo baada ya kutolewa kwa kadi nyekundu baadaye. 

Kwa ushindi huo, Simba itasubiri kukutana na mshindi kati ya wenyeji Mbao FC na Yanga SC zinazomenyaa kesho Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza. 

Katika mchezo huo uliochezeshwa na refa Mathew Akrama wa Mwanza, Azam FC ilipata pigo dakika ya 15 baada ya kiungo wake mchezeshaji, Salum Abunakar ‘Sure Boy’ kutolewa kwa kadi nyekundu ya moja kwa moja baada ya kumchezea rafu mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Hajib.

Ilionekana kama wachezaji hao wamegongana kwa kawaida mno, lakini kwa namna Hajib alivyojirusha huku akipiga yowe la kuugulia maumivu Akrama aliingia kwenye mtego wa kumtoa kwa kadi nyekundu Sure Boy. 

Tukio hilo lilileta kizaazaa kidogo uwanjani baada ya wachezaji wa Azam kumfuata refa na kuanza kumlalamikia kwa maamuzi yake. Walinzi wa Uwanja wa Taifa walimfuata Sure Boy na kujaribu kumtoa kwa nguvu, jambo ambalo liliwafanya wavutane na Meneja wa Azam, Philipo Alando. 

Mchezo uliendelea baada ya tukio hilo, huku timu zikiendelea kushambuliana kwa zamu na kabla ya Akrama kupuliza kipyenga cha kumaliza ngwe ya kwanza kukiwa hakuna bao. 

Kipindi cha pili, Simba walikianza vizuri na kufanikiwa kupata bao baada ya dakika tatu tu, kiungo Mohammed ‘Mo’ Ibrahim akimtungua vizuri kipa Aishi Salum Manula kwa shuti la mguu wa kulia kufuatia ya krosi ya mshambuliaji Mrundi, Laudit Mavugo. 

Simba wakaanza kucheza kwa tahadhari kwa kujihami zaidi baada ya bao hilo, huku Azam FC wakionekana kusaka bao la kusawazisha kwa nguvu zao zote. 

Mo Ibrahim akaonyeshwa kadi ya pili ya njano na kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 77 baada ya kumchezea rafu beki wa Azam FC, Shomary Kapombe. 

Beki Mkongo, Janvier Besala Bokungu akaizuia Azam FC kusawazisha baada ya kuokoa mpira uliopigwa kwa kichwa na Nahodha wa timu hiyo, John Raphael Bocco uliokuwa unaelekea nyavuni dakika ya 84. 

Kikosi cha Simba kilikuwa; Daniel Agyei, Janvier Bokungu, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Juuko Murshid, James Kotei/Said Ndemla dk88, Jonas Mkude, Shizza Kichuya, Muzamil Yassin, Laudit Mavugo/Mwinyi Kazimoto dk86, Ibrahim Hajib na Mohammed Ibrahim. 

Azam FC; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Gardiel Michael, Aggrey Morris, Daniel Amoah, Himid Mao, Stephan Kingue/Joseph Mahundi dk58, Shaaban Iddi/Frank Domayo dk46, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na Ramadhani Singano ‘Messi’/Mudathir Yahya dk82.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad