AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Kanda ya Pwani wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Frederick Sumaye, alisema hayo jana alipozungumza kwenye Kongamano la Vijana wa Chadema (Bavicha) lililofanyika mkoani Geita.
Sumaye alisema katika mfumo wa demokrasia, serikali huwekwa madarakani na wapiga kura kwa kutekeleza matakwa yao kwa kufuata katiba, sheria za nchi, taratibu na hata desturi.
“Hao walioiweka serikali madarakani (wananchi) ndio wakubwa na wana haki ya kuiuliza serikali yao, Rais wao na mwingine yeyote mwenye madaraka. Baadhi yao wana haki ya kutofautiana kimawazo na viongozi wao walioko madarakani ikiwa ni pamoja na Rais,” alisema.
Alisema kwa msingi huo kutoa maoni yaliyotofautiana na alichokisema kiongozi wa serikali akiwamo Rais mwenyewe si usaliti, uhaini, uchochezi wala kukosa adabu.
“Kuna watakaomsifia sana, kuna watakaotoa ushauri wa tofauti na kuna watakaopinga na kuwa na msimamo tofauti na Rais na serikali yake, makundi yote matatu ni sahihi, hakuna msaliti wala mchochezi… ni vema yawepo kwa afya ya demokrasia.
“Kama wewe ni kiongozi na hutaki kusikia yale yaliyo kinyume na msimamo wako basi usipende pia kuyasikia na yale yanayokusifia sana.
“Leo vyama vya siasa vimezuia kufanya mikutano ya hadhara ili viwajulishe watu wavyotaka kuwajulisha. Bunge ambalo ndiyo hufanya kazi kwa niaba ya wananchi shughuli zao huzionyeshwi mubashara kama huko nyuma,” alisema
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK