DOGO Janja Amwagia Sifa Harmorapa..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Msanii wa bongo fleva mwenye 'hit song' ya 'Kidebe' Dogo Janja amefunguka kwa kusema anamkubali rapa chipukizi Harmorapa kwa kuonesha uthubutu wake katika muziki licha ya watu kumkatisha tamaa kwa kumwambia hajui kitu lakini hakurudi nyuma.

Dogo Janja amebainisha hayo kupitia kipindi cha eNewz kwa kudai kilichomfanya amkubali msanii huyo ni kutokana na kumuona ana moyo wa ujasiri wa kupambana muda wote katika kufikia mafanikio yake ya kimuziki bila ya kujali watu wanasema kitu juu yake.

"Harmorapa ni mtu ambaye nimetokea kumkubali mimi kama mimi ....Ni mtu ambaye amejaribu kuonesha uthubutu..Stape ambayo ameenda ndiyo imenifanya mimi nimkubali zaidi, alianza wimbo wa kwanza watu wakamtisha tamaa, vunja moyo lakini hakuvunjika moyo. 'Dude' la pili akajaribu halafu likawa kali mimi nikasema huyu anahitaji vitu vichache tu vya kuongezeka kwa kuwa anaonekana na moyo wa uthubutu na anapenda kujifunza zaidi". Alisema Dogo Janja

Pamoja na hayo Dogo Janja amesema siyo kweli kwamba Harmorapa anabebwa na 'kiki' kuliko muziki wake ila watu wenyewe ndiyo wanamfanya kituko ili azidi kuonekana 'kiki.'
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad