Irene Uwoya Alamba Shavu Nono...Ateuliwa Kuwa Balozi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


KAMPUNI ya simu za mkononi ya itel mobile Tanzania leo imetiliana saini na msanii wa Bongo Muvi, Irene Uwoya kuwa balozi wake atakayeitangaza kampuni hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja.


Akizungumza katika hafla hiyo Hafla hiyo iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam katika Hoteli ya Hhyatty Regency, Ofisa Habari wa Kampuni hiyo, Zwolle Fernando


“Sisi Itel Mobile Tanzania tumefanya makubaliano ya kushirikiana na  msanii Irene Uwoya ambaye atazitangaza bidhaa zetu kwa muda wa mwaka mmoja kuanzia sasa. Tunaamini kupitia yeye ataweza kuuunganisha Itel Mobie na Watanzania kwa ujumla wao.”


Aidha alifafafanua kuwa wanaamini jamii itafaidika kwa kupata elimu kuhusu bidhaa zao kupitia kwake watasaidiana nae hasa kwenye matukio ya kuonesha ukarimu kwa baadhi ya makundi ya jamii ambayo watayaendesha kupitia mpango wao uitwao Charity Event Programs na mengineyo.


“Sote tunafaham mchango wa Uwoya kwenye jamii, amekuwa akielimisha kupitia muvi zake, kwa kutambua hilo sisi itel tutashirikiana nae kikamilifu kuhakikisha jamii inakipata kile inachotarajia kukipata kutoka kwetu na kwake pia.alisema Fernando.


Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Itel Mobile Tanzania, Cooper Chen alielezea kampuni yao kwamba inajishughulisha na masuala ya teknolojia na uvumbuzi wa simu ambayo mpaka sasa inakadiliwa kufikisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake.


Na karibu kipindi cha mlongo mmoja kampuni hiyo imekuwa ikitamba kwa kusambaza bidhaa zake kwenye zaidi ya nchi 45 duniani kote na kwa kipindi cha mwaka wa 2016 kampuni hiyo iliuza zaidi ya simu milioni 50 barani Afrika na kushika nafasi ya kwanza kwenye tatu bora ya kampuni za simu zenye idadi kubwa ya mauzo ya bidhaa zake.     


“Tunazalisha bidhaa bora kwa sababu tunaamini kwamba tunawapatia wateja wetu bidhaa za mawasiliano zenye viwango vya juu na huduma ya kuridhisha,tunaisaidia jamii kuungana na jamii nyingine za kimataifa katika kushirikiana kuleta maendeleo na maisha bora zaidi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad