Mzee Yusuph anakutaka ufute nyimbo zake kwenye simu yako

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Aliyekuwa mfalme wa muziki wa taarab nchini, Mzee Yusuph amefunguka na kueleza kuwa watu wote walio na nyimbo zake kwenye simu zao wafute na kuacha kusikiliza ili kuepuka dhambi.


Katika mahojihano na kipindi cha Mitikisiko ya Pwani cha Times Fm, Mzee Yusuph ameelezea maisha yake ya ndoa, kidini na kiuchmi yalivyo kwa sasa ukilinganisha na hapo awali.


“Mimi nikikubali watu wacheze nyimbo zangu ina maana nimeruhusu dhambi tena ni bora nirudi kuimba muziki tena hivyo, watu wote waliokuwa na nyimbo zangu kwenye simu zao wafute na kuacha kusikiliza kuepuka dhambi,” amesema Mzee Yussufu.


Mzee Yussufu amesema yeye hayupo kwenye kundi lake la ‘Jahazi Modern Taarab’ kama baadhi ya watu wanavyodhani na wala hafuatilii kabisa kundi hilo.


“Nilitaka kulivunja Kundi la Jahazi lakini sheria za nchi haziruhusu nikaliacha na haya niliambiwa na Basata wenyewe. Vyombo vya bendi ya Jahazi havikuwa vya kwangu tulikuwa tunasaidiana na mabosi,” amesema.


Katika hatua nyingine Mzee Yusuph amesema maisha ya kiuchumi kwa sasa ni toufauti na kipindi alichokuwa anafanya muziki kwani hapo awali kwa wiki alikuwa anaweza kutengeneza milioni moja na nusu mpaka mbili ila sasa kushika laki tano au milioni inaweza kumchukua miezi miwili.


Ameongeza kuwa wake zake wanne bado anaendelea kuishi nao kama kawaida, na kuwa na wake ni jambo ambalo amehimizwa na sio amri, na kwa sasa wanamjua ni mtu wa namna gani na mambo yote yanaenda sawa hakuna hata mmoja anayefanya sivyo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad