JPM Avunja CDA, Wafanyakazi Kupangiwa Kazi Ofisi Nyingine za Serikali..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Rais John Magufuli amevunja Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA) na kuagiza mali na shughuli zote zilizokuwa zikifanywa na mamlaka hiyo zihamishiwe halmashauri ya manispaa ya Dodoma.

Rais Magufuli pia amevunja bodi ya CDA hivyo  aliyekuwa mkurugenzi  mkuu wa bodi hiyo, Paskasi Muragili atapangiwa kazi nyingine na ameagiza wafanyakazi wote wa mamlaka hiyo wahamishiwe Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma na ofisi nyingine za Serikali kadri inavyofaa.

Rais Magufuli amevunja CDA kwa kutia saini hati ya amri ya Rais ya kuivunja mamlaka hiyo.

Amesema ameamua kuivunja mamlaka hiyo na kuhamishia majukumu yake katika Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma ili kuondoa mkanganyiko wa utoaji huduma kwa wananchi uliokuwa ukisababishwa ma mgongano kati ya vyombo hivyo viwili.

Pia amesema ni kwa ajili ya kuendana na mahitaji ya sasa ambayo yamedhihirishwa kuwa hakuna haja ya kuwepo kwa CDA.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad