Kesi ya Scoripon Mtoboa Macho Yafikia Hatua Hii..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi inayomkabili Salum Njetwe maarufu ‘Scorpion’ imeshindwa kuendelea kusikilizwa kwa mara ya nne mfululizo baada ya wakili wa utetezi kushindwa kufika mahakamani.

Wakili huyo, Juma Nassoro ameshindwa kufika leo, Alhamisi katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kwa ajili ya kumtetea mteja wake, baada ya kuwa na kesi nyingine Mahakama Kuu.

Wakili  Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga ameiambia Mahakama kuwa alipewa taarifa na wakili huyo kuwa alikuwa na kesi nyingine Mahakama kuu kwa Jaji Wambura.

“Mheshimiwa hakimu,  mshtakiwa yupo mbele ya mahakama yako lakini nimepata taarifa kutoka kwa wakili wake kuwa yupo Mahakama Kuu kwa Jaji Wambura mbapo anasikiliza kesi , hivyo tunaiomba Mahakama yako itoe ahirisho la mwisho na kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya  kuendelea na ushahidi”Alidai Katuga.

Hakimu  Mkazi  Flora Haule , anayesikiliza shauri hilo amekubalia ombi la upande wa mashtaka na kuahirisha kesi hiyo hadi Juni 8, mwaka huu na mshtakiwa amerudishwa rumande kutokana na shtaka linalomkabili kutokuwa na dhamana kwa mujibu wa sheria.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad