Mheshimiwa Rais, Umechuma Janga. Gwajima Sio DUDE Ila George H.W. Bush ni DUDE..!!!

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mchuma janga hula na wakwao! Na tutakula wote tu, hamna ujanja.
Sasa kwakuwa umechokoza li dege lililotulia, sasa na wewe utulie tuli usikie sauti yake.

George H.W Bush anahusikaje na Acacia?

Nov.27,2014 Cecilia Jamasmie anaandika ,'African Barrick imebaki historia, imebadili jina kuwa Acacia mining.'
Moja kati ya malengo yake ilikuwa kuendeleza kazi zake North Mara na kuzalisha ounce 450,000 ndani ya miaka mitano kwa gharama ya chini ya dola 750 kwa ounce.

Jan.03,1997 Anton Chaitkin anaandika Inside story juu ya genge la Bush na Barrick Gold Corporation. Anasema;
☆ Barrick Gold ni shirika linalojihusisha na mikakati ya siri katika siasa za George H W Bush.
☆ Shirika hili lenye makao yake Canada ndio biashara pekee ya Bush iliyofahamika wakati huo.
☆ Shirika hili lilianzishwa na marafiki wa kisiasa wa Bush, Wawezeshaji wakubwa wa biashara za madawa ya kulevya, wafanyabiashara haramu wa silaha na watakatishaji wa fedha.
☆ Shirika ni kubwa, liko USA, Canada, South America: Argentina, Chile, Peru, Bolivia na Brazil. Lipo pia Africa.

Majina makubwa kwenye shirika ni ya kina nani?

1. George Herbert Walker Bush 
♨Baba yake alikuwa partner kwenye taasisi binafsi kubwa na yenye nguvu, ya kibenki - Brown Brothers Harriman.
♨Bush alikuwa makamu wa rais na chief kwenye operations za siri katika utawala wa Reagan (1981-89).
♨Bush alikuwa rais wa Marekani (1989-93).
♨Bush alikuwa chief lobbyist wa Barrick, mwanahisa na mshauri mkubwa wa heshima wa bodi ya kimataifa ya washauri wa Barrick.

2. Adnan Khashogi.
♨ Billionea wa saudi na mfanyabiashara haramu ya silaha .
♨Muanzilishi wa Barrick Gold Corp.
♨Maarufu sana kwa biashara yake haramu ya kuiuzia Iran silaha.

3. Peter Munk na 4. Brian Mulroney ; hawa ntawaacha kwa sasa.

Hili ni janga kwasababu kwao Magufuli hatoshi hata kwa breakfast;
Angalia hapa chini!

$ Uwekezaji mkubwa katika shirika ulifanywa na Khashogi na mapartner wake katika biashara haramu ya silaha. Wakati huo wakihangaika na biashara iliyojulikana kama 'guns and cocaine triangle' kati ya Iran - Israeli - na Nicaragua. 1986 biashara hii ilikuja kubumburuka na ikawa maarufu kama 'Iran - contra' scandal.

$ Bush na yeye aliingia kwenye shirika kwa staili yake. Mwaka 1986-87 Barrick Gold Corp ilinunua ardhi, mali ya serikali ya Marekani, yenye thamani ya zaidi ya dola billion 10 kwa dola million 63 tu, kwaajili ya uchimbaji wa dhahabu.
Hapa ni USA ukumbuke, na sio mandazi republic kama hii yakwetu.
Bush alipochaguliwa 1988 akawezesha utaratibu wa kupata hati miliki kwa ajili ya eneo hili.Utaratibu huu ulikuwa special kwaajili ya Barrick tu!

♀Bush alishirikiana bega kwa bega na CIA na FBI katika kujaribu kupindua Serikali ya Fidel Castro katika uvamizi uliopewa jina maarufu kama Bay of Pigs invasion.
Walitumia mgongo wa kampuni ya Zapata Oil Bush akiwa kama rais wa kampuni na baadae Zapata Offshore Bush akiwa kama mmiliki.
Hapa kuna Memo kibao za ushahidi.

Nov.22, 1963 Bush alishiriki katika mauaji ya J.F.Kennedy, rais wa Marekani wakati huo kwasababu tu alikataza ndege za Marekani kutumika kwenye Bay of Pigs invasion. Kennedy pia alistopisha rogue operations zote za CIA na FBI .

Bush amefanya maovu mengi mno! Ana links na shetani wa kila aina;
☞ wa Nazi.
☞ wafanyabiashara ya madawa ya kulevya.
☞ Wafanyabiashara haramu ya silaha.
☞ Wauaji - assassins 
☞ CIA
☞ FBI 
☞ Na taasisi nyingi za kijeshi sehemu mbalimbali ulimwenguni.
Bush hajazaliwa hapo chini ya mfereji kwamba unaweza kumtumbua hata ukiwa grocery!

Kwenye moja ya mkutano mkuu wa umoja wa mataifa, siku moja baada ya Bush kuhutubia, Marehemu Hugo Chavez, Mungu ailaze roho yake mahali pema, Anasema, “ Shetani alikuja hapa jana, na mpaka leo hii, hii meza niliposimama inanuka sulfur.” Kisha Chavez akapiga ishara ya msalaba halafu akaangalia juu akiweka mikono yake kama mtu anayesali kumuomba Mungu.

Mdau unajua kwanini Chavez aliongelea harufu ya sulfur?

Chanzo - Jf
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad