AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Watu 12 wamethibitishwa kufariki na wengine 18 wamo katika hali mahututi hospitalini baada ya moto kuteketeza jumba la ghorofa 24 la makazi magharibi mwa London.
Moto huo ulizuka katika jumba hilo usiku wa kuamkia Jumatano. Jengo hilo bado linawaka moto na watu wengi hawajulikani walipo.
Taarifa za kwanza za kuzuka kwa moto jumba hilo la Grenfell Tower, kaskazini mwa Kensington ziliripotiwa saa, 00:54 BST (saa tisa kasoro dakika tisa Afrika Mashariki).
Watu 12 wamefariki kwa mujibu wa polisi, na idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka.
Kuna watu 78 ambao wamepokea matibabu hospitalini. Hospitali sita – St Mary’s, Chelsea and Westminster, Royal Free, St Thomas’, Charing Cross Hospital na King’s College Hospital – zilipokea majeruhi.
Kamishna wa wazima moto wa London Dany Cotton anasema wazima moto kadha walipata majeraha madogo.
Walioshuhudia wanasema huenda kuna watu waliokwama kwenye jengo hilo, lililokuwa na nyumba 120 za makazi.
Diwani wa Notting Dale Judith Blakeman, anayeishi hapo karibu, anasema kumekuwa na watu kati ya 400 na 600 ambao wamekuwa wakiishi katika jumba hilo.
Meya wa London Sadiq Khan amesema wazimamoto walifanikiwa kufikia ghorofa ya 12 pekee.
Polisi wa jiji wametoa nambari ya dharura kwa watu wanaotafuta habari kuhusu jamaa na marafiki – 0800 0961 233.
Source:BBC
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK