Yanga Yashindwa Kutamba Mbele ya Wekenya....Yatupwa Nje ya Mashindano

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MABINGWA wa Tanzania, Yanga wamekuwa timu ya mwisho ya nyumbani kuaga michuano ya SportPesa Super Cup baada ya kutolewa kwa penalti 4-2 kufuatia sare ya 0-0 ndani ya dakika 90 mchana wa leo Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Kwa matokeo hayo, Leopards itamenyana na mshindi kati ya Gor Mahia na Nakuru All Stars zote Kenya katika Fainali Jumapili na mshindi atajinyakulia dola za kimarekani 30,000 zaidi ya Sh. Milioni 65 na nafasi ya kucheza na Everton ya England Julai 13.

Kipa namba moja wa Yanga, Deogratius Munishi ‘Dida’ aliokoa mkwaju wa Marselas Ingotsi, lakini mlinda mlango wa AFC Leopards, Dennis Shika naye akacheza mikwaju ya Said Mussa na Said Juma ‘Makapu’.

Nahodha Nadir Haroub ‘Cannavaro’ na kiungo mshambuliaji Mzambia, Obrey Chira ndiyo pekee walifunga penalti za Yanga, wakati Bernard Mango, Allan Katerega, Duncan Otieno na Dennis Shika wakafunga za AFC Leopards.

Katika dakika 90 za kawaida za mchezo, timu zote zilimiliki mpira sawa, ingawa hakukuwa na mashambulizi ya kushitua.

Allan Kateregga wa AFC Leopards alipiga shuti kali dakika ya 39, lakini kipa wa Yanga, Dida akadaka. Kiungo chipukizi wa Yanga, Yussuf Mhilu alipiga shuti zuri dakika ya 43, lakini beki wa AFC Leopards, Joshua Mawira akaokoa.

AFC Leopards wakapoteza nafasi nyingine baada ya Vincent Oburu kushindwa kutumia pasi ya Ingotsi kwa kupiga shuti dhaifu lililodakwa na Dida. Chirwa naye akapiga krosi nzuri dakika ya 60, lakini mpira ukatoka nje.

Chipukizi Maka Edward Mwakalukwa naye akapiga nje dakika ya 62 baada ya kupokea pasi ya Juma Mahadhi.

Kikosi cha Yanga kilikuwa: Deogratius Munishi ‘Dida’, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Juma Abdul, Mohammed Ally, Andrew Vincent ‘Dante’, Pato Ngonyani/Babu Ally Seif dk61, Juma Mahadhi, Maka Edward/Said Juma dk76, Obrey Chirwa, Yussuf Mhilu/Samuel Greyson dk53 na Emmanuel Martin/Said Mussa dk56.

AFC Leopards: Dennis Shika, Otieno Ian, Marcus Abwao/Mike Kibwage dk88, Joshua Mawira, Salim Abdallah, Duncan Otieno, Mango Bernard, Allan Kateregga, Vincent Obura, Yakubu Ramadhani na Gilbert Fiamento/Marselas Ingotsi dk56.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. TAJA WEWE KWANZA JINA LAKO, NDIPO NA YEYE ATAMTAJA , CHADEMA MMEISHIWA, HAMNA NGOMA WALA NYIMBO.......HAPA KAZI TU!

    ReplyDelete

Top Post Ad