Afya ya Robert Mugabe Utata Mtupu....Adaiwa Kufichwa Hospitalini Nchini Singapore

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe, yuko nchini Singapore kwa ajili uchunguzi wa afya yake, huku maofisa wa serikali wakikanusha taarifa za kiongozi huyo kuzidiwa,

Kwa mujibu wa gazeti la serikali la Sunday Mail Rais Mugabe aliondoka nchini humo Ijumaa wiki iliyopita kuelekea nchini Singapore kwa matibabu na kwamba kiongozi huyo anatarajiwa kurejea katikati ya wiki hii.

Safari za rais Mugabe nchini Singapore zimeongezeka kwenye miaka ya hivi karibuni ambapo mara ya mwisho kuwa nchini humo ilikuwa ni mwezi Mei ambapo pia alisafiri kwa sababu za kimatibabu na mwaka 2011 na 2014 alifanyiwa upasuaji wa jicho.

Afya ya Rais Mugabe imeendelea kuzua mijadala nchini mwake ambapo mwezi Machi mwaka huu mamlaka nchini humo ziliwakamata waandishi wa habari wawili walioandika kuwa afya ya kiongozi huyo imezorota.

Licha ya umri alionao, chama chake cha ZANU-PF mwaka jana kilimteua kupeperusha bendera ya chama hicho kwenye uchaguzi mkuu ujao, huku kukiripotiwa mgawanyiko ndani ya chama hicho.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad