AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Msimu huo mpya wa Vpl wa mwaka 2017/2018 wenye jumla ya timu 16 unaanza kwa michezo saba kuchezwa katika viwanja tofauti.
Mabingwa wa michuano ya Kombe la Shirikisho (Azam Sports Federation Cup) na Ngao ya Jamii, Simba SC leo itatupa karata yake ya kwanza kwa kuwavaa Ruvu Shooting, wakati michezo mingine itakayo pigwa ni Ndanda FC dhidi Mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, huku Mwadui FC ikikipiga na Singida United.
Michezo mingine ni Mtibwa Sugar itakayocheza na Stand United, Kagera Sugar dhidi ya Mbao FC, Njombe Mji FC ikitarajia kutupa karata yake ya kwanza kunako Ligi Kuu dhidi ya Tanzania Prisons wakati mchezo wa mwisho ni vijana wa Manispaa ya Mbeya timu ya Mbeya City ikiingia dimbani kukipiga dhidi ya Majimaji FC ya Songea.
Wakati Mabingwa wa kihistoria wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara Dar es salaam Young Africans ikatarajia kuingia uwanjani hapo kesho Agosti 27 mwaka huu kumenyana na Lipuli FC.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK