Kufuatia Sakata la Shamba la Sumaye Waziri Lukuvi Aamua Kumjibu Haya Sumaye

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Kufuatia  Sakata la Shamba la Sumaye Waziri Lukuvi Aamua Kumjibu Haya
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe William Lukuvi amesema mtu yoyote asiyelipa kodi ya ardhi na kuendeleza ardhi hiyo, ni sababu tosha ya kunyang'anywa ardhi hiyo pamoja na kufutiwa hati ya umiliki kwa kuwa anaingizia hasara serikali

Waziri Lukuvi amebainisha hayo ikiwa imepita siku moja tokea kwa aliyekuwa Waziri Mkuu wa awamu ya tatu, Mh. Fredrick Sumaye kudai chanzo cha kupokonywa shamba lake ni siasa tu za yeye kuhama chama cha CCM na kwenda kuupa nguvu upinzani.

Akiongea kuhusu mashamba na viwanja kuchukuliwa Waziri Lukuvi amesema,
"Kila mtu atambue iwe ni kiwanja au shamba kama unatabia ya kutolipa kodi ya ardhi ni sababu tosha ya wewe kunyang'anywa shamba lako au ardhi unayomiliki".
Akiendelea kuongea Waziri Lukuvi amesema
"Imejitokeza kwa watu wachache kuchukua ardhi kubwa kwa miaka mingi kuliko hata uwiano wa uendelezaji wa ardhi hiyo, kwa mfano kuna hati moja hapa ambayo inapigiwa kelele tokea mwaka 1939 imekuwa ikitembea mikono mwa watu. Sasa miaka ile watu walikuwa wachache unapokwenda kuchukua ardhi ya kijiji hekari elfu 60 kwa mfano hivi sasa wananchi utakuwa umewaachia kitu gani?"
Pia Waziri Lukuvi amesema imekuwa kawaida ya baadhi ya watu wanapowahi maeneo  huwa wanakimbilia kuchukua sehemu zenye manufaa makubwa kwa upande wao na mwishowe wanashindwa kuendelezaa maeneo hayo kama walivyoyakimbilia.

"Unawahi kuchukua sehemu zenye manufaa kama mto, ardhi inayolimika, sasa unachukua hekari zote hizo halafu huliendelezi mwishowe shamba hilo hilo tunalikuta Benki umelikopea fedha. Kisha umepata fedha hizo unakwenda kujengea 'apartment' sehemu nyingine na kule wananchi wanalimezea mate.Serikali wanatumia nguvu kubwa sana kutuliza wananchi wasivamie hilo shamba , halilimwi, serikali hatupati kodi", alisisitiza Lukuvi.
Kwa upande mwingine, Waziri Lukuvi amesema serikali imekuwa na huruma kwa miaka mingi kwa wananchi wake lakini serikali ya uongozi huu wamekubaliana kila mtu afuate sheria anazo paswa kuzifuata.

----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Greedy ndio tatizo kubwa la watu wanaopata fursa za kupata uongozi.Kumiliki
    Heka 326 zenye rutuba kwaajili ya kuweka ngombe na kondoo 200 kwa zaidi ya miaka 15 is pathetic. Kwa idadi hiyo ya mifugo 10% ya eneo hilo ingetosha kabisa. Sumaye akae kimya.

    ReplyDelete
  2. Tena Baba Zeroanasema au anajisifu Kaenda Upinzani kuwapa nguvu!!! Ukweli yeye ..Hapeleki wala Harudishi Yupo Zero Balance sana sana ikizidi anaua UPINZANI. Fedeliki amka baba Hapa ni Kazi Tu.

    ReplyDelete

Top Post Ad